Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA Aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji wa Chankorongo utawekewa vituo vya kuongeza kasi ya maji ili upate uwezo wa kutoa huduma katika maeneo mengi zaidi Jimboni Busanda?

Supplementary Question 1

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile mradi huu wa Chankorongo ulioko Ziwa Victoria unaweza tu kupita katika vijiji alivyovitaja; je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba maji kutoka Ziwa Victoria yanaweza kufika kwenye maeneo ya Nyarugusu, Bukoli na Kata ya Nyakamwaga? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Magessa, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa eneo la Nyarugusu, maeneo ya machimbo haya Serikali tayari tuko kwenye mpango wa kupitisha mradi mkubwa pale wa maji kutoka Geita na utapita eneo hilo maji yanayotoka Ziwa Victoria na eneo lile pia, watapata extension kwa maana ya mtandao wa mabomba, maji yatafikia hapo na vilevile nipende kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge namna ambavyo waliweza kuzungumza na Mheshimiwa Waziri alipokuwa ziara katika eneo lake, basi yale mazungumzo yamezingatiwa kama ambavyo umeona tayari Meneja yule aliweza kubadilishwa na sasa hivi yupo Meneja mwingine ambaye yupo tayari kuendana na kasi ya Wizara hivyo, eneo la Nyarugusu pia litapata maji.

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA Aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji wa Chankorongo utawekewa vituo vya kuongeza kasi ya maji ili upate uwezo wa kutoa huduma katika maeneo mengi zaidi Jimboni Busanda?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya maji ya Busanda inafanana kabisa na changamoto ya maji iliyoko Korogwe Mjini. Nimekuwa nikifuatilia kwa Mheshimiwa Waziri na ameniahidi tatizo la Korogwe litatatuliwa na mradi wa miji 28 ambao Korogwe ni sehemu ya mradi huo.

Je, Serikali inawaahidi vipi wananchi wa Korogwe kwamba lini mradi huu utatekelezwa ili kuweza kutatua changamoto ya maji ambayo inawakabili wananchi wa Korogwe Mjini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alfred Kimea, Mbunge wa Korogwe Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nipende kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu amekuwa ni mfuatiliaji mzuri na nimeshaweza kuongea naye mara kadhaa na kumhakikishia eneo lake kupata maji na uzuri Korogwe Mjini ipo ndani ya ile miji 28 ambayo fedha tayari zipo na muendelezo wa maandalizi unaendelea na hivi karibuni kuanzia mwezi Aprili miji ile 28 shughuli za kupeleka maji zinakwenda kuanza mara moja.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA Aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji wa Chankorongo utawekewa vituo vya kuongeza kasi ya maji ili upate uwezo wa kutoa huduma katika maeneo mengi zaidi Jimboni Busanda?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona niulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mradi huu wa Busanda unafanana sana na ule mradi uliopo Wilaya ya Ubungo, hasa mradi wa 2f2b, unaoanzia Changanyikeni, Chuo Kikuu mpaka Bagamoyo na hasa ujenzi wa tanki kubwa la lita milioni sita pale Tegeta A, Kata ya Goba. Je, mradi huu utakamilika lini ili wananchi wote wa Kata ya Goba wapate maji safi, salama na yenye kutosheleza?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtemvu kutoka Kibamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi yote hii ambayo tayari utekelezaji wake unaendelea Wizara tunasimamia mikataba na namna ambavyo mkataba unamtaka yule mkandarasi kukamilisha mradi ule. Mheshimiwa Mbunge ninakupa uhakika kwamba tutasimamia kwa karibu na mradi ule utakamilika ndani ya muda ambao tumeupanga.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA Aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji wa Chankorongo utawekewa vituo vya kuongeza kasi ya maji ili upate uwezo wa kutoa huduma katika maeneo mengi zaidi Jimboni Busanda?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mradi wa maji wa Wilaya ya Muleba ambao unalenga kusaidia kata sita ambao umefanyiwa usanifu tangu mwaka 2018. Je, Wizara itaujenga lini na utakamilika lini kwa ajili ya kuwahudumia wakazi wa Wilaya ya Muleba?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daktari, Mbunge kutoka Muleba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu ambao usanifu wake umekamilika nao tayari Wizara tunaendelea na michakato kuona kwamba mradi huu tunakuja kuutekeleza ndani ya wakati.

Waheshimiwa Wabunge pale tunaposema kwamba, maji ni uhai, Wizara tunasimamia kuhakikisha kuona kwamba, wananchi wote wanaenda kupata maji safi na salama ya kutosheleza kwa lengo la kulinda uhai wa wananchi. Hivyo, Mheshimiwa Daktari nikuhakikishie kwamba, namna usanifu umekwenda vizuri na utekelezaji wake nao unakuja vizuri namna hiyo.