Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 9 Water and Irrigation Wizara ya Maji 123 2021-02-12

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA Aliuliza:-

Je, ni lini Mradi wa Maji wa Chankorongo utawekewa vituo vya kuongeza kasi ya maji ili upate uwezo wa kutoa huduma katika maeneo mengi zaidi Jimboni Busanda?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tumaini Bryceson Magessa, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji wa Chankorongo unatumia maji ya Ziwa Victoria ukiwa na pampu yenye uwezo wa kuzalisha lita 155,000 kwa saa ambapo kwa sasa unatoa huduma kwa wakazi wapatao 23,756 wa vijiji vitano vya Chankorongo, Chikobe, Nyakafulo, Chigunga na Kabugozo katika Jimbo la Busanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha mradi huu unanufaisha wakazi wengi wa Jimbo la Busanda, Serikali imeanza upanuzi wa mradi huo wa maji kwa kuanza utekelezaji wa Mradi wa Maji Katoro-Buseresere wenye thamani ya shilingi bilioni 4.2. Kupitia mradi huo wakazi wa vijiji vya Luhuha, Nyakagomba, Inyala na Mji Mdogo wa Katoro watanufaika na huduma ya maji. Kwa sasa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 20 na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Aprili, 2021.

Aidha, katika kuhakikisha wananchi wengi wananufaika na huduma ya maji, Serikali kupitia programu ya Mpango wa Malipo kwa Matokeo inaendelea na ujenzi wa miradi ya maji ya bomba katika vijiji vya Nyakagwe na Rwamgasa ambapo wakazi wapatao 14,315 wa vijiji hivyo watanufaika na huduma ya maji safi.