Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE Aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Daraja la Mto Mbaka linalounganisha Jimbo la Busokelo na Rungwe litakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Serikali nataka kufahamu ni hatua gani za kinidhamu zinazoweza kuchukuliwa na Serikali kwa wataalam wetu wanaosababisha variation ya miradi kuwa na gharama kubwa, kwa mfano, daraja hili la Mbaka ambalo limechukua muda mrefu sana. Kuna kitu tunaita geotechnical investigation hakikufanyika na ndiyo maana imechukua muda mrefu zaidi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa daraja hili litakapokamilika kutakuwa kuna madaraja mawili, kutakuwa kuna daraja hili ambalo linajengwa pamoja na lililokuwepo la chuma.

Je, Serikali ipo tayari kulichukua hili daraja la chuma kupeleka katika mto huo huo Mbaka lakini kwa kuweza kuunganisha kati ya Majimbo ya Busokelo, Kyela pamoja na Rungwe katika Kijiji cha Nsanga? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Atupele Mwakibete, Mbunge wa Busokelo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tayari ni utaratibu wa Serikali pale ambapo mfanyakazi yeyote amefanya kinyume na utaratibu anachukuliwa hatua na kwa sababu umakini huo ndiyo maana ilionekana kwamba daraja hili lilikosewa design na ikafanyiwa redesign na tayari ujenzi unaendelea kwa hiyo ni utaratibu wa kawaida pale panapotokea tatizo hatua zinachukuliwa.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, anauliza endapo daraja la chuma lililokuwepo litakwenda kwenye daraja lingine alilolisema ni utaratibu wa Serikali kwamba madaraja haya ya chuma ni madaraja ambayo yanatumika kwa ajili hasa ya dharura. Kwa hiyo utaratibu utawekwa kama itaonekana ni muhimu liende hapo litakwenda lakini vinginevyo tunayatunza maeneo ambayo ni ya kimkakati ili kunapotokea tatizo la dharura basi hayo madaraja yatakwenda hapo. Ahsante.