Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 112 2021-02-11

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE Aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa Daraja la Mto Mbaka linalounganisha Jimbo la Busokelo na Rungwe litakamilika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Fredy Atupele Mwakibete, Mbunge wa Busokelo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Daraja la Mto Mbaka ambalo lipo katika barabara ya Katumba - Lwangwa - Tukuyu yenye jumla ya kilometa 81, linaunganisha Halmashauri ya Busokelo na Mji wa Tukuyu. Barabara hiyo ni ya mkoa na inahudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Mheshimiwa Spika, hapo awali daraja hili lilikuwa la chuma (Bailey) lakini kwa kuzingatia umuhimu wa daraja hilo lililopo kwenye maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa mazao ya kilimo na mazao ya misitu, Serikali iliamua kulijenga kwa kiwango cha zege kuanzia mwaka 2018. Hata hivyo, wakati ujenzi ukiendelea kulijitokeza changamoto kadhaa ikiwa ni pamoja na usanifu ambao ilibidi urudiwe kuendana na hali halisi ya eneo husika. Usanifu huo ulikamilika mwezi Oktoba, 2019.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Mkandarasi anaendelea na utekelezaji wa ujenzi wa daraja hilo ambapo kazi za ujenzi zimefikia asilimia 68 na kazi zinatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2021. Ahsante.