Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA Aliuliza:- Serikali ilifanya upembuzi yakinifu na kubaini kuwa jumla ya shilingi Bilioni 21 zinahitajika ili kukarabati miundombinu ya maji Mji wa Tukuyu:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha na kuanza ukarabati wa miundombinu hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. ANTON A. MWANTONA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Wizara ya Maji. Nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwenye Mradi wa Maji Tukuyu nimeridhika, lakini kuna mradi mwingine ambao unaendelea katika Mji wa Ushirika, Kata ya Mpuguso. Tenki tayari limeshajengwa, mabomba tayari yameshafika kwenye tenki, usambazaji wa maji bado kwa wananchi kwa muda mrefu. Naomba Wizara ituambie wananchi wa Rungwe lini itaanza kusambaza maji kwa wananchi wa Rungwe?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; tuna Kituo cha Afya cha Ikuti ambacho kina matatizo makubwa sana ya maji. Nilikuwa naomba Wizara iwaambie wananchi wa Ikuti, Jimbo la Rungwe, ni lini maji yatasambazwa hasa baada ya upembuzi yakinifu wa mradi ule kuonekana kwamba, ni milioni 100 tu ambayo itapeleka maji kutoka kwenye chanzo cha maji mpaka kwenye Kituo cha Afya cha Ikuti? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, Anton Albert Mwantona, Mbunge wa Rungwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi unaoendelea pale miundombinu yake imeshakamilika, imebaki tu usambazaji wa maji. Mheshimiwa Mbunge mradi ule unakwenda kukamilika wiki chache zijazo na maji yatafika mabombani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Kituo cha Afya cha Ikuti kupata maji, Mheshimiwa Mbunge Serikali tutalifanyia kazi na namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, ndani ya muda mfupi utekelezaji wake utakuja kufanyika.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA Aliuliza:- Serikali ilifanya upembuzi yakinifu na kubaini kuwa jumla ya shilingi Bilioni 21 zinahitajika ili kukarabati miundombinu ya maji Mji wa Tukuyu:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha na kuanza ukarabati wa miundombinu hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwanza nimpongeze Naibu Waziri wa Maji pamoja na Waziri wake kwa kuufuatilia Mradi wa Nyanghwale na hivi karibuni unaenda kukamilika, nawapongeza sana. Swali langu ni kwamba, kwa kuwa mradi huu unaenda kukamilika. Je, bajeti ijayo Serikali imejipanga vipi kwenda kuweka mpango wa kusambaza maji kwenye kata zifuatazo: Kata ya Busolwa, Nyanghwale, Ijundu, Kakola, Shabaka na Mwingilo. Je, Wizara imejipanga vipi kwenda kusambaza maji hayo kwenye bajeti ijayo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Amar, Mbunge wa Nyanghwale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuweka mipango mahususi kuhakikisha mradi ule ambao tayari upo kwenye utekelezaji kwenye hatua za mwisho unakwenda kukamilika.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA Aliuliza:- Serikali ilifanya upembuzi yakinifu na kubaini kuwa jumla ya shilingi Bilioni 21 zinahitajika ili kukarabati miundombinu ya maji Mji wa Tukuyu:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha na kuanza ukarabati wa miundombinu hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Suala la maji la Tukuyu linalingana kabisa na matatizo ya maji katika Jimbo la Makambako. Mambo ya upembuzi yakinifu yalishafanyika. Je, Serikali ina mpango gani kupeleka maji au kutatua tatizo la maji katika Mji wa Makambako kwa sababu, tumekuwa tukiwaahidi watu kwa muda mrefu, ni lini sasa mradi ambao tumekuwa tukiwaambia wananchi utaanza kutekelezwa? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Makambako ni moja ya miji 28 ambayo inakwenda kunufaika na mradi ule mkubwa ambao tumeshapata fedha kutoka Benki ya Exim. Hivyo, Serikali inakwenda kuanza kutekeleza miradi hii yote ndani ya miji 28 ifikapo mwezi Aprili. Mheshimiwa Deo Sanga mradi wa maji Makambako nao ni sehemu ya miradi ya miji 28 hivyo kufikia mwezi Aprili wataalam wetu pamoja na wakandarasi watafika site kuanza kazi.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA Aliuliza:- Serikali ilifanya upembuzi yakinifu na kubaini kuwa jumla ya shilingi Bilioni 21 zinahitajika ili kukarabati miundombinu ya maji Mji wa Tukuyu:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha na kuanza ukarabati wa miundombinu hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza niishukuru sana Wizara ya Maji kwa sababu Jimbo letu la Temeke maji yamefika karibu kila kata. Tatizo letu kubwa ni kwamba bomba lile kubwa limepita katika barabara kubwa lakini kuvuta maji kwenda ndani ya nyumba zetu ambapo miundombinu siyo mizuri sana kwenye Kata za Buza na Kilakala na nyumba ziko mbali. Niombe Wizara ya Maji tunapoomba kuvutiwa maji ndani ya nyumba zetu, fedha ile ambayo tunatakiwa kuilipa kidogo ni kubwa, sasa mfikirie tuweze kuvuta kwa nusu ya bei halafu muendelee kutudai ndani ya malipo ya kila mwezi kama vile tunavyofanya luku ili tuweze kuona kila mmoja sasa anapata maji ndani ya nyumba yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. Tulia Ackson

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU SPIKA: Hilo ni ombi, nadhani utakuwa umeliandika Mheshimiwa Waziri.