Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 100 2021-02-10

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA Aliuliza:-

Serikali ilifanya upembuzi yakinifu na kubaini kuwa jumla ya shilingi Bilioni 21 zinahitajika ili kukarabati miundombinu ya maji Mji wa Tukuyu:-

Je, ni lini Serikali itatenga fedha na kuanza ukarabati wa miundombinu hiyo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Albert Anton Mwantona, Mbunge wa Rungwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha wananchi wa Mji wa Tukuyu wanapata huduma ya maji safi na salama ya kutosha, Serikali imeendelea na mikakati ya muda mfupi na mrefu. Mkakati wa muda mfupi ulihusisha uboreshaji wa chanzo cha maji cha Masalala, ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 200,000 pamoja na ulazaji wa bomba kuu lenye urefu wa mita 750. Kazi hizo zimesaidia kuimarisha huduma ya maji kwa wakazi wa Mji wa Katumba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa mkakati wa muda mrefu wa kuboresha hali ya upatikanaji wa maji safi katika Mji wa Tukuyu, Serikali kwa kutumia wataalam wa ndani wa Mamlaka za Maji na Usafi wa Mazingira za Mbeya na Tukuyu inafanya mapitio ya usanifu wa mahitaji kwa ajili ya uboreshaji wa huduma ya maji katika Mji wa Tukuyu kwa kutumia chanzo cha Mto Mbaka. Kulingana na usanifu kazi zilizopangwa kutekelezwa katika mradi huu ni pamoja na ujenzi wa bomba kuu la kilometa 15.5, ujenzi wa bomba la usambazaji maji kilometa 20, ujenzi wa tenki lenye ujazo wa lita 2,000,000. Mradi huu utatengewa fedha katika mwaka wa fedha 2021/2022 na utekelezaji wake unatarajia kuanza mwezi Julai, 2021.