Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE Aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji wa Nyashimo, Kata ya Nyashimo ambao ulitegemewa kukamilika mwezi Oktoba, 2020 utakamilika ili wananchi waweze kupata maji safi na salama?

Supplementary Question 1

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali na niipongeze Serikali kwa namna inavyochukua hatua juu ya mradi ule. Pamoja na hayo mradi ule katika Kijiji cha Mwagulanja umeacha sehemu kubwa sana ya wananchi wa Isuka takriban kilometa nne kufikia point ambapo maji yamewekwa.

SPIKA: Mheshimiwa swali lako ni Nyashimo…

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika, ni Kata ya Nyashimo sasa hicho Kijiji nilichokisema. Naomba tu kuuliza Serikali nini mpango sasa wa kufanya extension kutoka kwenye ule mradi kwenda kwenye Kijiji cha Mwagulanje kule Isuka ili wananchi wa kule nao waweze kupata maji? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Simon Lusengekile, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, huu mradi unaendelea kutekelezwa. Extension ni kazi ambayo hata yule Meneja aliyeko pale anaweza kufanya, kwa hiyo nimwaminishe Mheshimiwa Mbunge kwamba kufika mwezi Machi, tutaanza kuzitekeleza extension, lakini kwa kutumia wataalam wetu ambao wako kule.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE Aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji wa Nyashimo, Kata ya Nyashimo ambao ulitegemewa kukamilika mwezi Oktoba, 2020 utakamilika ili wananchi waweze kupata maji safi na salama?

Supplementary Question 2

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kyerwa kuna changamoto kubwa ya maji na hasa Kata za Kibale, Bugomora na Mrongo ila ninavyoongea hapa Kijiji cha Mgorogoro kuna tanki kubwa la maji ambalo tangu limewekwa…

SPIKA: Ni wapi huko unakokuulizia?

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, Kata ya Kibale.

SPIKA: Kata hiyo iko kwenye Wilaya gani?

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kyerwa, Jimbo la Kyerwa. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, tanki limewekwa kama urembo halijawahi kutoa maji. Kila siku wananchi wakiona habari za maji wananitumia message na sasa wamenikumbusha. Ni lini lile tanki katika Kijiji cha Mgorogoro litaanza kutoa maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anatropia kuhusu tenki kubwa lililokamilika lakini halitoi maji. Mkakati wa Wizara ni kuona kwamba miradi hii ambayo miundombinu imekamilika kufikia mwezi wa tatu kwenye Wiki ya Maji tunataka kuona kwamba maji yanatoka.

Mheshimiwa Spika, nimuahidi Mheshimiwa Anatropia kwamba nitafika huko Kyerwa na kuona nini kinasababisha maji hayatoki. Lengo ni kuona kwamba maji yanapatikana bombani. (Makofi)