Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 70 2021-02-08

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE Aliuliza:-

Je, ni lini Mradi wa Maji wa Nyashimo, Kata ya Nyashimo ambao ulitegemewa kukamilika mwezi Oktoba, 2020 utakamilika ili wananchi waweze kupata maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Jimbo la Busega, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji Nyashimo ulianza kutekelezwa mwezi Julai, 2019 na ulitegemewa kukamilika tarehe Oktoba, 2020 kwa gharama ya shilingi bilioni 1.58. Wakati utekelezaji wa mradi, Mkandarasi alipata changamoto zilizosababisha kuomba kuongezewa muda na hivyo mradi huu unatekelezwa kufikia mwaka huu 4 Aprili, 2021 ambapo ombi lake lillikubaliwa.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa utekelezaji wa mradi huo upo katika hatua ya majaribio ya kusukuma maji kupeleka kwenye tanki baada ya kufanikiwa kufunga umeme tarehe 9 Januari, 2021. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Aprili, 2021 na kuhudumia wakazi wapatao 12,000. (Makofi)