Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Chuo cha FDC kilichoko Shirika la Elimu Kibaha ambacho hakina vifaa vya kujifunzia, karakana zimechoka pamoja na miundombinu mibovu?

Supplementary Question 1

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Spika, ahsante nafikiri hata wewe umeshangaa ukiwa kwenye kiti hicho hicho mwaka jana nilisimama mbele yako nikiuliza kwa nini chuo hiki hakifanyiwi ukarabati na ilijibiwa na Wizara ya Elimu mpaka mwaka jana ilikuwa haijulikani kama chuo hiki kiko chini ya Wizara ya Elimu au TAMISEMI, walipeleka Wizara ya Elimu pesa ya chakula wakaenda kuwanyang’anya wakasema kwamba chuo hiki hakiko chini ya Wizara ya Elimu na mpaka tunavyoongea saa hizi watoto wa shule pale hawana chakula sasa hivi tunajibiwa na TAMISEMI ina maana mpaka sasa hivi ndiyo imejulikana kwamba chuo hiki kiko chini ya TAMISEMI.

Sasa swali je, ni lini chuo hiki kitapata ruzuku ya chakula kwa sababu makusanyo yao ni madogo sana?

La pili, ni lini majengo na miundombinu ya chuo hicho yatafanyiwa uboreshaji?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ni kweli Mheshimiwa Mbunge amekuwa akifuatilia suala hili na fedha zilipelekwa pale, hiki chuo kiko chini ya TAMISEMI, kwa hiyo ilipogundulika kwamba fedha zimepelekwa pale na Wizara ya Elimu, ikabidi zirudishwe zipelekwe kwa malengo yaliyokuwa yamekusudiwa. Lakini nimesema kwamba chuo hiki kimeshafanyiwa tathmini, tumepeleka fedha pale milioni 70 kwa mapato ya ndani kwa maana ya kupunguza shida iliyopo, lakini tunaendelea kutafuta fedha zikipatikana wakati wowote hata leo kitaanza kufanyiwa ukarabati huo mkubwa wala hamna shida.

Mheshimiwa Spika, lakini swali lake la pili anauliza habari ya chakula, hili naomba nilipokee tulifanyie kazi kwa sababu utaratibu ni kwamba wanafunzi wote ambao wapo maeneo yote nchi nzima wanaosoma lazima wapewe chakula na tunapeleka fedha ya chakula kulingana na idadi ya wanafunzi katika eneo hili na hawezi kukaa shuleni bila kuwa na chakula.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba niahidi kwamba hili tutalifanyia kazi mapema iwezekanavyo liweze kufanyiwa kazi kama kweli ni tatizo katika eneo hilo.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Chuo cha FDC kilichoko Shirika la Elimu Kibaha ambacho hakina vifaa vya kujifunzia, karakana zimechoka pamoja na miundombinu mibovu?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, wote tunatambua lengo kubwa la vyuo hivi ni pamoja na kuondoa ujinga lakini vilevile kufanya watu waweze kujiajiri wenyewe na lengo kubwa nilikuwa na mimi nashangaa ni kwa sababu gani what is the uniqueness ya hiki chuo mpaka hiki kiwe chini ya Wizara ya TAMISEMI wakati tunajua vyuo vyote vya maendeleo vilikuwa chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na vyote vikapelekwa Wizara ya Elimu.

Sasa nataka kujua what is uniqueness yaani nini upekee wa chuo hiki kuwa chini ya TAMISEMI wakati tunajua Wizara ya Elimu ndiyo ingeweza zaidi kuhakikisha kwamba vinajengewa labda hata hizi changamoto zisingekuwepo? Nilitaka kujua hilo.

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri, TAMISEMI kwa majibu yake mazuri kuhusiana na swali hili.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Susan Lyimo kama ifuatavyo; ni kweli kwamba vyuo vyote vya maendeleo ya wananchi viko chini ya Wizara yangu na Wizara imekuwa ikivifanyia ukarabati vyote 54 ambavyo viko chini ya Wizara na hapa katika majibu ya msingi Mheshimiwa Naibu Waziri ameelezea historia ya hicho chuo. Lakini historia inaweza ikabadilika, naomba kama Serikali tulipokee hilo wazo tuangalie ni namna gani hiki chuo kinaweza tukakifanyia utaratibu ili kiweze kupata huduma vizuri zaidi kama ambavyo vyuo vingine 54 vinapata huduma. (Makofi)