Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 45 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 376 2019-06-13

Name

Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Chuo cha FDC kilichoko Shirika la Elimu Kibaha ambacho hakina vifaa vya kujifunzia, karakana zimechoka pamoja na miundombinu mibovu?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mary Deo Muro, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (Kibaha Folk Development College -KFDC) kilianzishwa mwaka 1964 kikijulikana kama Farmers Training Centre kwa ufadhili wa Serikali ya Norway chini ya Mradi wa Tanganyika Nordic Project. Baada ya mradi huu kukabidhiwa kwa Serikali ya Tanzania mwaka 1970, jina la mradi lilibadilika na kuitwa Shirika la Elimu Kibaha na hivyo chuo kikawa chini ya Shirika hili. Mwaka 1975 wakati huo Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi vilipoanzishwa nchi nzima, chuo hiki kilianza kuitwa Kibaha FDC chini ya Wizara ya Elimu kikiwa miongoni mwa vyuo 55 nchini. Kwa kipindi kirefu chuo hiki hakijafanyiwa ukarabati mkubwa, hata hivyo, kupitia mapato yake ya ndani chuo kimekuwa kikifanya ukarabati mdogo mdogo.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kupitia Chuo Kikuu cha Ufundi cha Dar es Salaam (DIT) imekifanyia chuo tathmini na kuandaa mpango mkubwa wa ukarabati. Vilevile chuo kiliandaa andiko la mradi na kuomba fedha kutoka Serikali ya Uholanzi ili kuboresha chuo ambapo vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 70 vilipatikana na kusaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa vifaa chuoni.

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango wa kukarabati chuo hicho utakaotekelezwa kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.