Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE (K.n.y. MHE. MOSHI S. KAKOSO) aliuliza:- Wilaya ya Tanganyika haina Jengo la Polisi Makao Makuu ya Wilaya. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi eneo la Makao Makuu ya Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa Wilaya ya Tanganyika ni jiografia yake ni ngumu sana na Makao Makuu ya Wilaya yako Majalila, lakini OCD anakaa Mishamo na ukizingatia jiografia ile ni pana sana, watu wa Karema wanashindwa kwenda Mishamo.

Je, Serikali itaweka mikakati gani kuhakikisha basi kile kituo cha polisi hata kama bado fedha hazijapatikanika, lakini kituo kiwekwe center ili watu wote katika Wilaya ile waweze kujua kituo chao cha polisi kiko wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kutokana na jiografia mbaya ya Wilaya ya Tanganyika, je, ni lini Serikali itatuletea magari ya polisi kwa ajili ya patrol kwa sababu kuna misitu mingi, mikubwa sana katika wilaya ile, sasa majambazi wako wengi na uhalifu unafanyika mara kwa mara. Serikali itatuletea lini magari kwa ajili ya patrol ya Wilaya yetu ya Tanganyika? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani hoja ya Mheshimiwa Lupembe ni ya msingi, na kwa kuzingatia msingi wa hoja yake, sasa tutalifuatilia kwa karibu tuone lile eneo ambalo Halmashauri imekusudia kulitenga kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi, liwe Majalila kama ambavyo amependekeza ambapo ni Makao Makuu ya Wilaya. Sambamba na ule ujenzi wa nyumba nne ambazo mchakato wake unaendelea wa ujenzi katika eneo hilo la Wilaya ya Tanganyika, liende sambamba pamoja na rai ambayo Mheshimiwa Mbunge ametoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusianana na magari nayo, kwa sasa hatuna magari mapya ambayo yameingia, lakini kwa kutambua umuhimu wa jiografia ya Tanganyika kama alivyoeleza Mheshimiwa Mbunge, basi suala lake tumelichukua na pale ambapo magari yatapatikana basi tutazingatia.