Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 43 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 362 2019-06-11

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE (K.n.y. MHE. MOSHI S. KAKOSO) aliuliza:-

Wilaya ya Tanganyika haina Jengo la Polisi Makao Makuu ya Wilaya.

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi eneo la Makao Makuu ya Wilaya?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Mpanda Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Tanganyika ni miongoni mwa Wilaya mpya zilizoanzishwa na Serikali katika miaka ya hivi karibuni ambazo hazina vituo vya polisi na hata nyumba za kuishi askari.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua hitaji la Kituo cha Polisi katika Makao Makuu ya Wilaya ya Tanganyika na mpango wa kujenga Vituo vya Polisi katika Makao Makuu ya Wilaya yataanza mara baada ya kufanyika kwa tathmini ya eneo husika.