Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rukia Ahmed Kassim

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RUKIA KASSIM AHMED aliuliza:- Baadhi ya magereza nchini yamejaa wafungwa na mahabusu ambao ni wakimbizi. Je, ni lini Serikali itawarejesha wakimbizi hao makwao ili kupunguza msongamano ndani ya magereza yetu?

Supplementary Question 1

MHE. RUKIA KASSIM AHMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini bado nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wakimbizi kutoka Somalia pamoja na wakimbizi kutoka Ethiopia, hawawezi kuingia nchini mpaka wapitie nchi ya Kenya. Je, Serikali haioni kwamba ipo haja kwa kushirikiana na nchi ya Kenya kuwazuia wakimbizi hawa wasiingie katika nchi yetu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa ukiacha wakimbizi walioko katika magereza, kuna wakimbizi ambao wako katika kambi za wakimbizi. Kwa mfano, Kadutu - Kigoma, Ulyankulu - Tabora pamoja na kambi nyingine. Wakimbizi hawa wana tabia ya kuzaana sana na kwa kweli idadi yake inaongezeka ukizingatia miaka 10 iliyopita sasa hivi wako mara mbili zaidi.

Je, Serikali, kwa kuwa nchi zao tayari zina amani, wana mkakati gani wa kuwarejesha wakimbizi hawa ili wasiendelee kuzaana hapa? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na rai yake ya kwanza, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba rai yake ambayo ameitoa tumeshaanza kuifanyia kazi. Hivi karibuni tulikuwa tuna kikao kilichoshirikisha ngazi ya Mawaziri wa Tanzania, Kenya na Ethiopia, ili kujadiliana namna ya pamoja ya kudhibiti wimbi la wahamiaji hawa hususan wanaotokea Ethiopia ambao wanaingia kwa wingi kupitia Kenya na jambo hilo limeleta mafanikio makubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusu suala la wakimbizi kurudi makwao, kama ambavyo nimejibu swali langu la msingi kwamba kwa takwimu za mpaka Aprili, 2019 tuna zaidi ya wakimbizi 99,000 ambao wameamua kurudi kwa hiari. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba nalo hili ni jambo ambalo tumeshaanza kulifanyia kazi na tunaendelea nalo. Kwa sababu ni kweli kama alivyozungumza Mbunge kwamba hali ya amani katika nchi hizi imetulia, hakuna sababu ya wakimbizi hawa kuendelea kubaki katika nchi yetu kwa kipindi hiki.