Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH M. MASABURI Aliuliza:- Nchi yetu imejaliwa kuwa na rasilimali nyingi zikiwemo bahari, maziwa, mito na mabwawa mengi ya asili pamoja na rasilimali watu kubwa ambao hawana ajira. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha vijana na akina mama kwenye kila Halmashauri nchini kutenga maeneo maalum ya kujenga mabwawa ya kufugia samaki ili makundi hayo yapate kujiajiri?

Supplementary Question 1

MHE. JANETH M. MASABURI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuweza kuniruhusu niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue fursa hii kuipongeza TAMISEMI kupitia Mawaziri wake wote kwa kazi nzuri wanayoifanya hapa nchini. Tumekuwa tukiwaona wanatekeleza wajibu wao ipasavyo, lakini katika eneo hili la vijana na wanawake ninaomba niulize maswali kama yafuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa vijana wengi na wanawake hapa nchini wameshindwa kufanya biashara zao kwa tija kutokana na ukosefu wa ujuzi na maarifa wa kufanya biashara hizo. Je, Serikali iko tayari kuiwezesha kutoa mafunzo makundi haya ya ufugaji wa samaki ya uhakika na kwa idadi kubwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa, sekta ya uvuvi imeonesha kuwa na fursa kubwa ya kukuza ajira, kukuza kipato, kuboresha lishe na hata kuiingizia Serikali fedha za kigeni. Je, Serikali iko tayari kuanzisha mpango wa kujenga vizimba pembezoni mwa maziwa na mabwawa na hata kandokando ya mwambao wa bahari?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru kwa pongezi ambazo ametutumia kwenye Ofisi ya TAMISEMI kwa kazi ambayo inafanyika tunamshukuru sana.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Masaburi ametoa maswali mawili, swali la kwanza anatuhimiza tuwe na mafunzo kwa vijana na akinamama na kweli hili jambo linafanyika, kwa sababu jambo la msingi ni kwamba tumeshatoa maelekezo kila Halmashauri ina maelekezo na baada ya kugundua kwamba kuna … pia na mafunzo … mtaji ndio maana Bunge hili tukufu likapitisha sheria kwamba kila Halmashauri itatenga mapato yake ya ndani asilimia nne kwa akinamama, nne kwa vijana na mbili kwa watu wenye mahitaji maalum au wenye ulemavu kwa hiyo hii pia ni sehemu ya mtaji.

Mheshimiwa Spika, lakini la pili kila Halmashauri ina Maafisa wa Ustawi wa Jamii na kuna Maafisa wa Vijana katika Halmashauri zote nchini. Naomba nitumie nafasi hii kuwaelekeza washirikiane na Maafisa wa Ugani kwenye Wizara ya Kilimo waende wakatoe mafunzo kwa vijana hawa na kimsingi hata ziara ambazo Mheshimiwa Waziri anafanya, Manaibu, Makatibu Wakuu na Wakurugenzi ndio tunaangalia miradi ambayo imeanzishwa na Halmashauri na kukagua ikiwepo ni pamoja na ufugaji wa samaki katika maeneo yetu.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba tupokee ushauri wake tuwasiliane na viongozi wenzetu wa Wizara ya Uvuvi. Tutalifanyia kazi, ahsante sana.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. JANETH M. MASABURI Aliuliza:- Nchi yetu imejaliwa kuwa na rasilimali nyingi zikiwemo bahari, maziwa, mito na mabwawa mengi ya asili pamoja na rasilimali watu kubwa ambao hawana ajira. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha vijana na akina mama kwenye kila Halmashauri nchini kutenga maeneo maalum ya kujenga mabwawa ya kufugia samaki ili makundi hayo yapate kujiajiri?

Supplementary Question 2

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, katika Jimbo langu la Ngara tumehamasisha vijana wanaosoma vyuo vikuu nchi nzima wanaotoka Wilaya ya Ngara kwa ajili ya kuweka umoja na ushirika na miaka miwili mfululizo wamekuwa wakija kujitolea wakati wa likizo ndefu kufundisha kwenye shule zetu za sekondari na tayari wamesajili shirika lao linaitwa Mzalendo Education Organisation (MEO). Serikali iko tayari kuwashika mkono ili kusudi waweze kuendelea kutengeneza mazingira ya ajira kwa vijana wenzao kwa sababu tayari Halmashauri imeshawapatia ekari 10 kwa ajili ya kuanza miradi ya mfano.

Je, Serikali wako tayari kuweza kuwashika mkono ili vijana hawa wawe mfano kwa vijana wenzao nchi nzima? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kuunganisha vijana katika eneo lake na kuwapa mawazo haya ambayo ni mawazo mema kweli kweli. Ni kweli, tupo tayari na utayari wetu umeshaanza kutekelezwa. Naomba nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ngara na Afisa Elimu pale waende katika eneo hili wakutane na vikundi hivi vya vijana, wazungumze nao halafu walete maoni ni kitu gani hasa wanataka kusaidiwa ili waweze kufanya kazi hii nzuri ambayo imeanza. Ahsante sana.