Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 42 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 346 2019-06-10

Name

Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH M. MASABURI Aliuliza:-

Nchi yetu imejaliwa kuwa na rasilimali nyingi zikiwemo bahari, maziwa, mito na mabwawa mengi ya asili pamoja na rasilimali watu kubwa ambao hawana ajira.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha vijana na akina mama kwenye kila Halmashauri nchini kutenga maeneo maalum ya kujenga mabwawa ya kufugia samaki ili makundi hayo yapate kujiajiri?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Maurice Masaburi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kupitia Mpango wa Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili Halmashauri zote nchini zimeelekezwa kutenga maeneo ya ardhi kwa ajili ya kuchimba mabwawa ya kufugia samaki, kuendeleza ufugaji wa samaki kwenye vizimba na kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali kwa ajili ya uzalishaji bora na endelevu wa samaki.

Mheshimiwa Spika, jitihada zetu nyingine za Serikali za kuwasaidia wavuvi nchini wakiwemo vijana na akinamama ni kuondoa kodi katika zana za malighafi yaani uvuvi kwa engine za kuvulia, nyavu, kufuta Kodi ya Ongezeko la Thamani yaani VAT kwenye engine za kupachika, nyuzi za kushonea nyavu na vifungashio ili kupunguza gharama za zana na vyombo vya uvuvi na kutoa ruzuku kwenye zana za uvuvi ambapo mvuvi anatakiwa kuchangia asilimia 60 na Serikali ni asilimia 40.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri zote nchini zimekuwa zikipewa mafunzo ya uvuvi endelevu kwa wavuvi wakiwemo vijana na akinamama kupitia semina, warsha, vipeperushi, makala, redio na luninga kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi na wadau mbalimbali. Pia Maafisa Uvuvi katika Halmashauri zote nchini wamepatiwa mwongozo wa ugani katika sekta ya uvuvi kwa lengo la kutoa elimu kwa wavuvi na ukuzaji wa viumbe kwenye maji na kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambapo jumla ya nakala 1,000 zilisambazwa.