Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza:- Shule za watoto wenye mahitaji maalum hupokea wanafunzi wenye matatizo mbalimbali kama vile ulemavu wa viungo, viziwi, uoni hafifu na wenye ualbino; baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwatekeleza wototo wao wakishawapeleka kwenye shule hizo:- (a) Je, ni kwa nini Serikali haitoi fedha kwa shule hizo iliziweze kuhimili mahitaji ya watoto hao? (b) Je, ni kwa nini Serikali inaziachia majukumu Halmashauri kuendesha shule hizo wakati zinapokea wanafunzi kutoka nje ya mkoa?

Supplementary Question 1

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali yangu mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, watoto hawa wanapopelekwa kwenye shule wazazi wao wanawatelekeza, hawafuati watoto wao kuhakikisha kwamba wanapata mahitaji maalum hasa mavazi. Siyo hiyo tu, shule hizo zinakosa pesa za kulipia walinzi, kulipa, maji, kulipa mapato na Matron na wengine wanahitaji misaada maalum na hasa wale wenye uoni hafifu au wasiyoona.

Je, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu sasa kuwepo na mpango maalum wa kuhakikisha kwamba watoto hawa fedha hizo zinapelekwa kwa kuzingatia kwamba Halmashauri hazina mapato, zimezinyang’anywa mapato yote, haziwezi kuhimili kumudu kusaidia shule hizo; Kuwepo na mkakati maalum wa kuhakikisha kwamba huduma kama hizo zinapatikana kwa watoto hawa.

Mheshimiwa Spika, shule ambazo mimi nimeuliza swali ni za Serikali, sikutegemea kwamba Serikali inaweza ikakosa takwimu maalum kwa ajili ya kuweza kutoa huduma.(Makofi)

Je, Serikali inataka kutuambia kwamba inafanya kazi bila kuwa na takwimu sahihi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Swali lake la kwanza Mheshimiwa Conchesta amezungumza hoja ambayo kimsingi inatakiwa Watanzania wote tuichukue na kuifanyia kazi. Ni kweli kwamba wako wazazi ambao wametelekeza watoto wao, hata akimpeleka shuleni, anamwacha pale moja kwa moja, hawezi kumfuatilia.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli ni jambo hili ni jukumu la kijamii, haliwezi kuwa la Serikali peke yake, tulichukue na tuwashauri kwamba hawa ni watoto wenye haki sawa na watoto wengine, tuwapokee, tuwakubali, na tuwasaidie. Tukishikamana sisi Watanzania na jamii kwa ujumla na Serikali, jambo hili litakuwa jepesi sana.

Mheshimiwa Spika, vile vile Mheshimiwa Conchesta anapendekeza kwamba kama kuna uwezekano wa kupeleka fedha zaidi, tufanye hivyo. Ninachokizungumza hapa, tunapeleka huduma kwenye shule kulingana na idadi ya wanafunzi kulingana na taarifa tuliyopokea hapa. Hili swali nalijibu kwa pamoja na swali lake la pili. Tunapozungumza kwamba taarifa hazipatikani, kama alivyosema mwenyewe ni kwamba kuna watoto wengine wanafichwa katika jamii, kuna wengine kweli hawako kwenye mfumo rasmi, kuna wengine wapo mashuleni, lakini taarifa ya Serikali Kuu hapa TAMISEMI pamoja na Hazina ambao wanatuma fedha moja kwa moja kwenye mashule, tunapata taarifa kutoka kwenye Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, katika jambo hili natoa wito kwa Waheshimiwa Wabunge, Madiwani, Viongozi wa Vijiji na Mitaa, tupatieni taarifa sahihi. Tukipata taarifa sahihi, tutapeleka fedha kwa kiwango kinachotosha katika eneo lile; na hiyo ndiyo ambayo inakosekana hapa. Kwa hiyo, jambo hili ni la kwetu wote, tunaendelea kufanya kazi. Inawezekana kuna upungufu katika maeneo mbalimbali, tumetembea katika shule mbalimbali, lakini kuna upungufu, lakini kadri Serikali inavyopata uwezo imekuwa ikiimarisha huduma hizi.

Mheshimiwa Spika, tumesema hakuna mtoto ambaye atakufa katika shule hii au kupata shida kubwa bila kupata huduma. Cha muhimu tusaidiane, Mheshimiwa Mbunge kule wa Kagera ameona taarifa ipo, tuwasiliane, tutaipokea, tutalifanyia kazi. Lengo ni kuhakikisha kwamba watoto hawa wanapata elimu na ushahidi upo kwamba huko watoto waliachwa, walitelekezwa, wamechukuliwa na Serikali na wasamaria wema, wameingia kwenye mfumo rasmi, sasa hiivi ni viongozi wakubwa katika nchi hii, wamejiajiri na wanasaidia wenzao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza:- Shule za watoto wenye mahitaji maalum hupokea wanafunzi wenye matatizo mbalimbali kama vile ulemavu wa viungo, viziwi, uoni hafifu na wenye ualbino; baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwatekeleza wototo wao wakishawapeleka kwenye shule hizo:- (a) Je, ni kwa nini Serikali haitoi fedha kwa shule hizo iliziweze kuhimili mahitaji ya watoto hao? (b) Je, ni kwa nini Serikali inaziachia majukumu Halmashauri kuendesha shule hizo wakati zinapokea wanafunzi kutoka nje ya mkoa?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa katika Mkoa wa Dar es Salaam kumekuwa na ongezeko la watoto wenye mahitaji maalum; na kwa kuwa shule ambazo zinapokea watoto wenye mahitaji maalum kama Majimatitu Maalum, Mtoni Maalum, Salvation Army, Wailesi Maalum, Uhuru Mchanganyiko, Mgulani Inclusive na Sinza Maalum zinakuwa hazitoshelezi mahitaji, watoto wale bado wanabaki majumbani:-

Je, Serikali haioni haja sasa ya kuongeza katika shule zote za msingi vitengo vya watoto wenye mahitaji maalum ili nao waweze kupata elimu katika maeneo yao wanayotoka? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Mariam Kisangi kwa mawazo haya mazuri ya kuunga mkono Serikali ya Chama cha Mapinduzi. Naomba nitoe taarifa kwamba sasa hivi baada ya kuona kwamba unapotenga shule maalum ni kama wale watoto unawatenga, wanakuwa isolated sana katika mazingira yao. Kwa hiyo, sasa hivi tumekuja na kitu kinaitwa Elimu Jumuishi. Ndiyo maana tumetoa maelekezo nchi nzima, tunapojenga miundombinu mipya, hata kama ni Kituo cha Afya izingatie mahitaji maalum, kama ni shule zetu za msingi na sekondari ziwe na mahitaji maalum.

Mheshimiwa Spika, ukienda kule Buhangizo utawakuta, Chaibushi utakuwata, Kilosa Sekondari utawakuta. Kwa hiyo, hiyo imeshaanza. Cha muhimu, ametoa warning, tuendelee kuzingatia. Tumeendelea kuwaeleza wanafunzi wa kawaida kwamba hawa watoto wenye mahitaji maalum ni wenzao, wawapokee, wawakubali, wawasaidie na wasome kwa pamoja pale inapowezekana. Hilo kwa kweli linafanyika. Cha muhimu hapa tutaongeza nguvu zaidi na kwa maoni ya Mheshimiwa Mbunge tutayafanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, ahsante.