Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 40 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 332 2019-05-31

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza:-

Shule za watoto wenye mahitaji maalum hupokea wanafunzi wenye matatizo mbalimbali kama vile ulemavu wa viungo, viziwi, uoni hafifu na wenye ualbino; baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwatekeleza wototo wao wakishawapeleka kwenye shule hizo:-

(a) Je, ni kwa nini Serikali haitoi fedha kwa shule hizo iliziweze kuhimili mahitaji ya watoto hao?

(b) Je, ni kwa nini Serikali inaziachia majukumu Halmashauri kuendesha shule hizo wakati zinapokea wanafunzi kutoka nje ya mkoa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge wa Viti Maalum, lenye vipengele (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, wanafunzi wenye mahitaji maalum wana haki sawa ya kupata elimu kama wanafunzi wengine wasio na mahitaji maalum. Kwa kutambua changamoto wanazokutana nazo wanafunzi hawa, Serikali kupitia mpango wake wa elimu bila malipo, imekuwa ikigharimia huduma za chakula kwa wanafunzi wote wenye mahitaji maalum wanaosoma katika shule za bweni na za kutwa. Vilevile Serikali imekuwa ikinunua vifaa na visaidizi kwa kadri ya upatikanaji wa fedha kisha kuvigawa kwa wanafunzi husika.

Mheshimiwa Spika, kwa kipindi cha mwaka 2015/2016 hadi 2018/2019, Serikali imetumia jumla ya shilingi bilioni 3.87 kwa ajili ya chakula kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu shuleni. Changamoto kubwa kwenye utaratibu huu ni upatikanaji wa takwimu sahihi za wanafunzi wenye mahitaji maalum kutoka kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa na Serikali inaendelea kuimarisha mfumo wa upatikanaji na utoaji wa takwimu sahihi za wanafunzi wenye mahitaji maalum. Serikali itaendelea kusimamia utoaji bora wa elimu kwa wanafunzi wote wakiwemo wenye mahitaji maalum bila kujali mkoa au eneo ambalo anatoka.

Mhehimiwa Spika, ahsante.