Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:- Suala la kupima na kupanga Miji ni jukumu la Serikali:- (a) Je, Kwanini Serikali isije na mkakati endelevu wa kupanga Miji yote ambayo imetangazwa kwenye gazeti la Serikali? (b) Je, kwanini Serikali inatoa hoja nyepesi kwamba kazi ya kupima na kupanga Miji ni kazi ya halmashauri wakati inajua kwamba halmashauri nyingi nchini hazina nguvu ya kifedha kufanya kazi hiyo? (c) Mji wa Kasulu ni mkongwe; je, ni lini Serikali itasaidiana na Halmashauri ya Mji wa Kasulu kupanga Mji huo?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona nina maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, kwanza sijui kama wewe kwako kule Kongwa umesalimika. Miji mingi inageuka kuwa Miji holela, kuwa squarter kwa sababu haipimwi, haipangwi na halmashauri nyingi hazina fedha ya kufanyakazi hiyo, ndiyo ulikuwa msingi wangu wa swali sasa nina maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hii interim plan ya Kasulu ya 2008 mpaka 2018 mwenyewe kwenye jibu lake Mheshimiwa Waziri anakiri kwamba iliishia njiani haikukamilika na taarifa nilizonazo ni kwamba mpango huu haukukamilika, sasa swali la kwanza; Je, sasa Mheshimiwa Waziri madam wewe mwenyewe uko hapo Je, ni lini sasa mtakuja kukamilisha hiyo Land use planning ya Kasulu ili ikamilike? Maana iliisha tu 2018 haikukamilika 2018.

Mheshimiwa Spika, swali la pili; katika Miji 18 ambayo Waziri umeitaja Je, katika Miji hiyo ambayo itakuwa katika hiyo program ya kuendeleza na kupanga Miji Je, Mji wa Kasulu umo? Na kama Mji wa Kasulu haumo ni lini utakuwemo kwenye program hiyo? Suala la miji ni suala kubwa sana, kubwa sana vinginevyo Miji itakuwa squarter yote katika nchi yetu. Ahsante sana.

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, namshauri Mheshimiwa Nsanzugwanko aongee na Halmashauri ya Kasulu ili waonesha mahitaji ya master plan maana yake ukihitaji unaanza kwenye Kamati ya Mipango Miji na halmashauri yenyewe ya Wilaya inaonesha uhitaji wa kuwa na master plan ya Wilaya yake. Wakishaazimia hivyo, basi waweke bajeti kwenye halmashauri yao ya kufanya master plan ya Mji wao wa Kasulu na Miji yote.

Mheshimiwa Spika, sisi kama Wizara, wenye Miji yao maana mamlaka ya upangaji kwa mujibu wa Sheria ya Mipango Miji ni wenye Wilaya (halmashauri) ambao ni Madiwani. Sisi kama Wizara hatuwezi ku-dectate, hata matumzi ya ardhi wanaosimamia zaidi ni halmashauri yenyewe kwahiyo wakishaazimia kwamba sasa wanafikiri ni wakati muafaka watengeneze master plan basi waazimie vilevile na kuweka bajeti.

Mheshimiwa Spika, tunajua liko tatizo la wataalam wa halmashauri, hatuna wataalam wa kutosha wa Mipango Miji lakini serikali imechukua jitihada ya kutambua weledi na utaalam uliko Nchi hii kwa hiyo tumeanzisha Makapuni chini ya Bodi ya Mipango Miji Makampuni ambayo ya Watanzania wenye weledi na utaalam mkubwa wa kufanya hizi master plan ambayo Halmashauri zinaweza zikawatumia.

Mheshimiwa Spika, lakini halmashauri ambayo haina uwezo huo, Wizara inaweza kusaidia wataalam wa Wizara tulionao wachache kuja kushirikiana na halmashauri ile katika kutoa usimamizi wa utayarishaji wa master plan. Kwa hiyo, nakushauri Mheshimiwa Nsanzugwanko utakapokuwa tayari Manispaa ya Kasulu basi tushirikishe na sisi lakini kama hujui mahali pakuanzia tuzungumze mimi na wewe naweza nikamtuma mtaalam mmoja kule Kasulu akawaeleze wale Madiwani namna master plan inavyoweza kuandaliwa.

Mheshimiwa Spika, lakini katika mipango hii ya hizi master plan 18 zinazoandaliwa naomba Mheshimiwa Nsanzugwanko nimuombe nitamtajia Wilaya zote ambazo ziko kwenye huu mpango wa master plan kwenye bajeti yangu ijumaa na Waheshimiwa Wabunge wote watasoma lakini ijumaa nitawapeni pia nafasi ya kujua pamoja na Miji hii ya Wilaya mnayoijua, lakini viko vijiji vyenu wengine hamvijui vimeshaiva sasa ili kuzuia hizo squatter, vijiji vingine Wilaya imeshaamua kuvitangaza vimeletwa kwangu na nimeshavitangaza na vyenyewe vipangwe kimji ili watu wanaoishi katika vijiji hivyo wapangwe, wapimiwe na wapewe hati kama za Mjini navyo nitawapa jedwali ili Waheshimiwa Wabunge wote mjue vijiji vyenu ambavyo vina hadhi ya kimji ambavyo tumeshavitangaza Tanzania nitawapeni ijumaa nakushukuru. (Makofi)

Name

Freeman Aikaeli Mbowe

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:- Suala la kupima na kupanga Miji ni jukumu la Serikali:- (a) Je, Kwanini Serikali isije na mkakati endelevu wa kupanga Miji yote ambayo imetangazwa kwenye gazeti la Serikali? (b) Je, kwanini Serikali inatoa hoja nyepesi kwamba kazi ya kupima na kupanga Miji ni kazi ya halmashauri wakati inajua kwamba halmashauri nyingi nchini hazina nguvu ya kifedha kufanya kazi hiyo? (c) Mji wa Kasulu ni mkongwe; je, ni lini Serikali itasaidiana na Halmashauri ya Mji wa Kasulu kupanga Mji huo?

Supplementary Question 2

MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa Mheshimiwa Waziri na kwa sababu swali langu litafanana kidogo na swali la Kasulu linahusu Mji mdogo sio Mji mdogo, Mji wa Hai ambao zamani ukiitwa Bomang’ombe Makao Makuu ya Wilaya ya Hai.

Mheshimiwa Spika, mji huu ni Mji ambao unakuwa na kwa kasi kuliko pengine Miji yote katika Mkoa wa Kilimanjaro ukiwa ni mkoa ni Mji ambao unaunganisha Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha na Manyara kwa upande wa Simanjiro. Mji huu sasa hivi unakaribiwa kuwa na takribani na wakazi zaidi ya 100,000 na unahudumia eneo lenye viunga vya karibu watu 200,000 kuanzia Mkoa wa Manyara, Mkoa wa Arusha, Mkoa wa Kilimanjaro na ni get way to the Kilimanjaro international Airport ambapo ni karibu sana na uwanja wa ndege wa Kimataifa na of course ndio njia na lango la kuingilia katika Mlima Kilimanjaro ambao ni chanzo kikubwa sana cha mapato kwa Taifa letu.

Mheshimiwa spika, sasa Mji huu ukiacha barabara Kuu ya Lami inayotoka Arusha kwenda Moshi na inayotoka kwenye ene la Hai kwenda Sanyajuu katika Jimbo la Siha Mji huu hauna barabara hata moja ya lami. Sasa katika kupanga Miji ni pamoja na ujenzi wa barabara za lami ili ujenzi na upangaji miti uwe kamili ni lazima uendane vilevile na mitaro ya maji pamoja na ujenzi wa barabara za lami.

Mheshimiwa Spika, halmashauri zetu sasa hivi hazina uwezo wowote wa kuweza kufanya miradi mikubwa ya kiwango hiki. Na natambua hapo nyuma kidogo kulikuwa kuna program kuna project ya sustainable cities ambalo nafikiri limekuwa funded na World Bank ambayo ilichagua baadhi ya Miji ambayo kwa umuhimu wake wa kiuchumi iliweza kuwekewa miundombinu ya barabara za lami. Na hata Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni za 2015 Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli alitoa ahadi ya kujenga barabara kilomita 5 za lami ambazo kwa bahati mbaya bado tunazisubiri kwa hamu sana.

Mheshimiwa spika, sasa Mheshimiwa Waziri katika utaratibu huo wa kupanga Miji nini kifanyike ili Miji muhimu kama hii ambayo inahudumia watu wengi na ni sura ya Taifa inaweza kufanyika ili ipate lami? Nini kifanyike katika hiyo mipango Miji kuikamilisha kwa kujenga miundombinu ikiwemo barabara za lami? (Makofi)

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa spika, master plan haijengi miundombinu master plan ni dira ya kuonesha mahitaji ya mpango au mahitaji ya huduma ndani ya Wilaya. Master plan wenye Wilaya yenu mtapanga kutaka kujua barabara zipite wapi, maeneo ya mazishi ni wapi, maeneo ya makazi ni wapi, maeneo ya biashara na huduma mbalimbali. Kwa sababu hata mkiwa na fedha ya barabara kama hamna maeneo mliyopanga kujenga barabara hazitafanya kazi na ndio maana mnakuwa na hela halafu mnaamua kufanya vyovyote au mnavunja nyumba za watu hovyo. Kwa hiyo, la kwanza nakushauri Mheshimiwa Mbowe pangeni master plan ili muone uhitaji wa leo mnahitaji kuwa na barabara kiasi gani, za saizi gani, za lami na kila kitu na mahitaji mengine.

Mheshimiwa Spika, then mkishapanga master plan kuainisha maeneo hayo mtakuja kuyapima lakini baadaye sasa ndio mtawaomba sasa huduma mbalimbali na kuziwekea bajeti ili ziwemo kulingana na master plan iliyopo.

Kwa hiyo, nimelichukua ombi lako hilo, lakini nashauri kama nilivyosema kwa Mheshimiwa Mbunge mwenzangu wa Kasulu naomba halmashauri yako mkae kama council katika miradi kingi mnayobuni pale Hai basi mbuni utengenezaji wa master plan kama hamna mtu wa kuwaelekeza pale Moshi kuna Kanda na nimepeleka pale mtalaam mbobezi Afisa Mipango Miji Mkurugenzi Msaidizi wa Kanda mnaweza mkamualika yule bure akaja kuwapa maelekezo na utalaam wa awali wa namna ya kutayarisha master plan ya Hai ili iweze kuwaoneshea huduma zenu zipangwe namna gani katika Wilaya ya Hai.

Mheshimiwa spika, lakini hilo jingine ulilosema nakushauri kwa sababu Wizara ya TAMISEMI iko hapa Dodoma pengine ukipata fursa ungepita pale kwenye Ofisi za TAMISEMI ili angalau hayo majibu mengine ya lini zitajengwa hizo barabara uweze kujibiwa pale ofisini.