Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 38 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 322 2019-05-29

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:-

Suala la kupima na kupanga Miji ni jukumu la Serikali:-

(a) Je, Kwanini Serikali isije na mkakati endelevu wa kupanga Miji yote ambayo imetangazwa kwenye gazeti la Serikali?

(b) Je, kwanini Serikali inatoa hoja nyepesi kwamba kazi ya kupima na kupanga Miji ni kazi ya halmashauri wakati inajua kwamba halmashauri nyingi nchini hazina nguvu ya kifedha kufanya kazi hiyo?

(c) Mji wa Kasulu ni mkongwe; je, ni lini Serikali itasaidiana na Halmashauri ya Mji wa Kasulu kupanga Mji huo?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, heshima yako.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Nicodemus Nsanzugwanko, Mbunge wa Kasulu Mjini lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa mkakati wa kupanga Miji yote ambayo imetengazwa kwenye gazeti la Serikali kwa kuandaa mipango kabambe ya Majiji, Manispaa na Miji. Aidha, Serikali imeainisha upya maeneo yote ambayo yameiva kuendelezwa kimji kwa ajili ya kuyatangaza katika gazeti la Serikali kuwa maeneo ya mipango yaani planning areas na hivi sasa maeneo ambayo tumeshayatangaza kwamba yameiva kimji mtayaona kila Mbunge ataona kwenye bajeti yangu vijiji na maeneo ambayo yametangazwa kuiva kimji yanayofika 455.

(b) Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kifungu namba 7(1) na (5) cha Sheria ya Mipango Miji namba nanne ya Mwaka 2007, jukumu la kupanga na kupima Miji ni la mamlaka za upangaji ambazo ni Halmashauri za Majiji, Manispaa na Miji na mamlaka ya Miji midogo. Hata hivyo Serikali imeendelea kuzisaidia halmashauri kupanga na kupima Miji yao kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo. Kwa mfano, katika Mwaka wa Fedha 2018/2019 Serikali kupitia Wizara imetoa jumla ya shilingi bilioni 6.4 kwa halmashauri 29 kwa ajili ya upangaji, upimaji na umilikishaji wa ardhi. Aidha, inawezesha uandaaji wa mipango kabambe Miji 18 hivi sasa kupitia program ya kuzijengea uwezo mamlaka za Miji ambayo iko chini ya Ofis ya Rais, TAMISEMI.

(c) Mheshimiwa Spika, mwaka 2008 Serikali iliandaa mpango wa muda wa kati wa matumizi ya ardhi wa Mji wa Kasulu wa miaka 10 (2008 - 2018) ambao ulikuwa unatumika kuongoza na kusimamia uendelezaji wa mji huo wa Kasulu ambako ndiko Mheshimiwa Nsanzugwanko ni Mbunge wake. Mpango huo uliisha muda wake mwaka 2018 hivyo ni jukumu la Halmashauri ya Mji wa Kasulu kuanza mchakato wa kuandaa mpango mwingine kabambe wa kuongoza na kusimamia uendelezaji wa Mji wa Kasulu.