Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. KHADIJA NASSIR ALI) aliuliza:- Uzito mkubwa wa mwili ni dalili za mwanzo za magonjwa yasiyoambukiza:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupambana na magonjwa haya? (b) Je, mbali na mazoezi ni mbinu gani nyingine za kitaalamu za kupambana na vitambi?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa hapa amebainisha wazi kwamba kitambi kinasababishwa zaidi na vyakula vilivyopitiliza hasa vyenye wanga na kwa tamaduni zetu watanzania karibia vyakula vyote tunavyovitumia ni vya wanga. Je, Serikali inatushauri watanzania tule vyakula gani ili kuepukana na vitambi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini la pili, utakuwa ni shahidi kwamba sasa hivi kuna ongezeko kubwa sana la uzito uliopitiliza kwa watoto, vijana lakini hata kwa akinamama na hapa tunapozungumza hivyo vitambi pia hata kina mama wanavyo. Sasa tunataka tuone kwamba Serikali ina mkakati gani mahususi, hapa wamezungumzia habari ya chanjo lakini pamoja na hizo elimu wanazotoa, ni nini kifanyike ili tatizo hili lisiendelee kuathiri haswa malika haya madogo ambayo nimeyataja? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, wanga kwa nini ndiyo unaosababisha na Serikali ina ushauri gani? Kwa ruksa yako naomba niwakumbushe hatua za kibailojia kidogo Waheshimiwa Wabunge, wanga ni mzuri kwa mwili, lakini kazi ya wanga ni kuzalisha nguvu tu, unapoliwa ukapitiliza kwa wale ambao mnakumbuka somo ya biolojia wanga uliozidi unageuzwa kwenda kuwa complex compound inayoitwa glycogen haya ni mafuta. (Makofi)

Mheshimwia Spika, sasa glycogen katika mwili wa binadamu hasa mtu mzima hauna kazi nyingine yoyote isipokuwa ni kuhifadhiwa, na huu hii glycogen ambayo kiasili ni protini inahifadhiwa katika maeneo mbalimbali ya mwili wa binadamu ikiwa ni pamoja na mishipa ya kupitisha damu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana tunasema pamoja na appetite ambayo inaweza kukufanya ule ugali mwingi sana, lakini ni vizuri ukala kiasi kile ambacho kitakwenda kuzalisha energy kwa maana ya nguvu ya kuusukuma ule mwili wenyewe, unapokula ziada ndiyo huleta matatizo.

Sasa sisi ushauri wetu kama Serikali nini, kwanza ni kula ulaji ambao unazingatia mlo wenye tunaita mlo bora na hasa protini na katika upande wa protini pamoja na ubora wote wa protini za nyama, lakini protini iliyo bora zaidi ni ile protini inayotokana na mimea. Ushauri wetu Waheshimiwa Wabunge mle zaidi protini na hasa protini zinazotokana na mimea.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili Mheshimiwa Mbunge Rashid Shangazi anauliza nini kifanyike ili hili rika ambalo linaonekana linaathirika zaidi kama vile vijana na hata wakinamama amewataja. Sisi Serikali tunashauri, kwa kawaida kisayansi inakubalika kwa watu wazima kuwa ndiyo waathirika zaidi wa upatikanaji wa vitambi, wanapopata vijana ni jambo lisilokuwa la kawaida. Sasa vijana wanachoshauriwa ni kubadilisha lifestyle namna ya uendaji katika maisha, ulaji wa chipsi uliopitiliza, na unywaji wa pombe uliopitiliza haya ndiyo yanayopelekea matatizo haya…

SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri.

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, lakini na ufanyaji wa mazoei pia, ninashukuru.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. KHADIJA NASSIR ALI) aliuliza:- Uzito mkubwa wa mwili ni dalili za mwanzo za magonjwa yasiyoambukiza:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupambana na magonjwa haya? (b) Je, mbali na mazoezi ni mbinu gani nyingine za kitaalamu za kupambana na vitambi?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niiulize wali dogo la nyongeza. Kwanza nimpongeze sana mdogo wangu Ulega inaonekana shuleni alifanya vizuri kwenye somo la biolojia, na ni mfano mzuri nimefuata ule ushari wake ndiyo maana kitambi changu kimepungua. Serikali inajitahidi kupambana na magonjwa mbalimbali nchini hivi karibuni kuna ugonjwa wa homa ya Dengue ambao hali yake sasa ni mbaya na vimeanza kuripotiwa vifo kutokana na jambo hili. (Makofi)

Sasa Serikali inachukua hatua gani kwa kuhakikisha jambo hili linakwisha kwa sababu tukiendelea kulinyamazia vifo vitaendelea kuongezeka watu wanaendelea kumwa na hali ya Jiji la Dar es Salaam kwa sasa ni mbaya?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nape Moses Nnauye Mbunge wa Mtama kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa hapa karibuni imeibuka ugonjwa wa Dengue na hasa katika Jiji la Dar es Salam, Serikali inafahamu juu ya tatizo hili na imeanza kuchukua hatua za makusudi.

Mheshimiwa Spika, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote na watanzania. Moja katika jambo kubwa ililoligundua Serikali ni kuwa gharama kubwa zinazolipwa na watanzania wanaopata matatizo hayo katika sehemu za kutolea huduma za afya. Sasa katika Serikali jitihada inayofanyika hivi sasa ni kuhakikisha matibabu ya Dengue yanakuwepo na yanapatikana kwa bei zilizokuwa nafuu ili kuweza kuwasaidia watanzania. (Makofi)

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. KHADIJA NASSIR ALI) aliuliza:- Uzito mkubwa wa mwili ni dalili za mwanzo za magonjwa yasiyoambukiza:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupambana na magonjwa haya? (b) Je, mbali na mazoezi ni mbinu gani nyingine za kitaalamu za kupambana na vitambi?

Supplementary Question 3

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, mara nyingi tunaambiwa kwamba wale wanaotaka kupunguza mwili ama vitambi wanakatazwa kula aina ya nyama na badala yake wanaelekezwa kula samaki na nyama za kuku, lakini katika hizi nyama za kuku kuna hawa makuku kutoka nje ambao kama yanauzwa kama KFC ambayo yanamapaja kama watu, Mheshimiwa hebu tunataka ushahidi juu ya kuku hawa wa kizungu broilers hasa katika kuongeza vitambi. (Kicheko)

Je, hawana mahusiano ya moja kwa moja kuku hawa? Ahsante.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ulaji wa kuku broilers kwanza kuku ni katika protini na nimesema na nimesema katika jibu la msingi kuwa protini ni muhimu, protini ziko za aina inyotokana na wanyama na ile protini inayotokana na mimea. Lakini anataka uhakika ya kwamba broilers wanatatizo hilo la kuweza kumfanya mtu awe na kitambi au laa!

Mheshimiwa Spika, hakuna utafiti wa kisayansi unaokwenda kutupelekea kutuambia kuwa broilers wanashida katika afya ya wanadamu, jambo hili liko palepale, ulaji wa kupitiliza unaweza kukupelekea katika hayo matatizo. Lakini naomba niwahakikishie broilers hawana shida yoyote, kinachowafanya broilers wakue ni hormones, ambazo hormones kisayansi ni vitamins. Kwa hivyo sisi wanasayansi tunachokifanya vyakula vya broilers tunaweka vitamins za kutosheleza za kuhakikisha ukuaji wao unakuwa ni ukuaji wa haraka…

SPIKA: Ahsante sana.

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kulinganisha na kuku wa kienyeji.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. KHADIJA NASSIR ALI) aliuliza:- Uzito mkubwa wa mwili ni dalili za mwanzo za magonjwa yasiyoambukiza:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupambana na magonjwa haya? (b) Je, mbali na mazoezi ni mbinu gani nyingine za kitaalamu za kupambana na vitambi?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kunipa nafasi niulize swali langu. Nilikuwa napenda kuiuliza Serikali kwamba sisi tusiokuwa na vitambi tunakula vyakula vyote hivyo ambavyo Mheshimiwa Dkt. Ulega amevizungumza na hatujawahi kuona mabadiliko yoyote katika maumbile yetu. Je, Serikali inatushauri tule nini zaidi kwa sababu vya wanga, vinywaji vyote tumetumia bado tuko kwenye maumbile haya haya.

Je, Serikali inatushauri tule nini ili na sisi tubadilike tufanane na wao? (Kicheko)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, nataka kujua watu wa aina yake ambao miili yao haina shukurani kama ulivyoiita wafanyeje? Na yeye anataka kupata kitambi, namshauri Mheshimiwa Musukuma na yeye ikiwezekana apate kuwaona watalaam wa lishe nina hakika watampangia diet ambayo itampelekea na yeye kupata mwili anaouhitaji.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. KHADIJA NASSIR ALI) aliuliza:- Uzito mkubwa wa mwili ni dalili za mwanzo za magonjwa yasiyoambukiza:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupambana na magonjwa haya? (b) Je, mbali na mazoezi ni mbinu gani nyingine za kitaalamu za kupambana na vitambi?

Supplementary Question 5

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana nitaenda kwenye swali la msingi kuhusu non committable disease, 2016/2020 ulitengenezwa mkakati maalum kuhusiana na magonjwa yasiyokuwa ya kuambukizwa.

Je, mkakati huu wamagonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza ulikuwa ni kwa nchi nzima au ulikuwa ni pilot project? Na kama ni pilot project kwa maeneo gani?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, mkakati ulikuwa ni pilot ama ulikuwa ni wan chi nzima. Utafiti kwa kawaida huwa ni pilot unachukuliwa eneo moja halafu kwa njia labda kama ya sampling kisha matokeo yanatokana na eneo lile yanaweza kuwa ndio matokeo elekezi. Kwa hivyo naomba nimuhakikishie mama yangu kuwa kwa maelezo ziada ya matokeo ya utafiti huu uliofanywa niko tayari baada ya Bunge kuweza kuzungumza na wataalam wetu na kumtafutia zile takwimu na kuweza kumpatia.