Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:- Serikali imeziagiza halmashauri zote nchini kutenga asilimia tano ya vijana na asilimia tano ya wanawake kutoka mapato ya ndani ili kuchangia mfuko wa maendeleo wa wanawake na vijana:- Je, Serikali inachukua hatua gani kwa halmashauri ambazo hazizingatii takwa hilo?

Supplementary Question 1

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Serikali, lakini kwa umuhimu mkubwa sana wa suala hili, Serikali nimeuliza ni hatua zipi zinazochukuliwa, lakini Serikali imeniletea majibu kusema kwamba sheria imetungwa. Sheria tumeitunga sisi wenyewe Wabunge na tumeipitisha sisi wenyewe na imesainiwa na Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, lakini je, ni hatua gani zimechukuliwa? Ndiyo lilikuwa swali langu la msingi, lakini nasikitika kwamba halijajibiwa kwa sababu hakuna hatua amabazo zimeonyeshwa kuchukuliwa katika halmashauri ambazo hazitengi fedha hizi na ukizingatia kwamba fedha hizi zinasaidia maendeleo ya kiuchumi kule kwa yale makundi maalumu ambayo yametajwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba Serikali iweze kusema ni hatua zipi ambazo zimechukuliwa hasa baada ya Serikali ya kutungwa kwa sheria.

Mheshimiwa Spika, lakini pia, kwa kuwa zipo halmmashauri ambazo zina changamoto ya mapato, je, Serikali ina mkakati gani wa kuzisaidia halmashauri hizo ili ziweze kutenga asilimia 10 ya haya makundi ili waweze kuchochoe maendeleo? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza ni kweli alitaka kujua hatua, lakini nimesema kwenye jibu la msingi kwamba, sheria hizi na kanuni zimetungwa mwaka jana 2018 na mwaka huu wa bajeti tumepitisha fedha ambazo zinakwenda kwenye mwaka 2019/2020. Sasa hizi halamshauri ambazo zitashindwa kutekeleza sheria hii, baada ya sheria hii kuwa in place, tumetangaza kanuni wanazo, then hatua zitachukuliwa dhidi ya hawa watu ambao wamekuwa wakichukua hizi fedha. Kwa sababu mwanzoni sheria haikuwepo na kanuni hazikuwepo ilikuwa halmashauri inatenga kwa kujisikia. Hayo ndiyo majibu ya Serikali na Mheshimiwa Mbunge avute subira.

Mheshimiwa Spika, na maelezo ya nyongeza ni kwamba, kwa bahati nzuri halmashauri zote, mikoa yote na wakurugenzi, kwenye mwaka huu wa fedha wakati wa mjadala wa bajeti ya TAMISEMI, kila Mkurugenzi alikuwa anaji- commit kwamba anarudi kwa hii awamu ya robo ya nne ya mwisho, ni lazima wakamilishe kutenga fedha kwa kiwango tulichokubaliana na mwaka wa fedha wa bajeti ujao, kama kuna mkoa utakuja bila kukamilisha zoezi hili na niwaombe Waheshimiwa Wabunge kwenye ziara zetu katika majimbo na wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya, nendeni kwenye halmashauri, Wakurugenzi wawaonyeshe fedha zilizotengwa, vikundi vilivyokopeshwa, miradi ambayo imeanzishwa ili mtupe taarifa tuweze kuchukua hatua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, anauliza habari ya changamoto za mapato. Nimezungumza vilevile kwenye jibu la msingi, hata kama halmashauri inakusanya shilingi 100, imeelekezwa, ndani ya hicho ilichokusanya kidogo hicho, itenge asilimia 10 ya fedha hizo baada ya kuondoa mapato lindwa. Kwa hiyo, katika hoja hii na katika sheria hii na kanuni zetu, hakuna halmashauri ambayo itapata utetezi wa kwamba mapato ni ya chini. Hatukumlazimisha apeleke bilioni mbili, bilioni 10, bilioni 100, tumesema, 10% ya makusanyo ya mapato lindwa.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:- Serikali imeziagiza halmashauri zote nchini kutenga asilimia tano ya vijana na asilimia tano ya wanawake kutoka mapato ya ndani ili kuchangia mfuko wa maendeleo wa wanawake na vijana:- Je, Serikali inachukua hatua gani kwa halmashauri ambazo hazizingatii takwa hilo?

Supplementary Question 2

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Spika, ahsante, ukifuatilia trend ya utoaji wa hizi fedha za vikundi asilimia 10, mara nyingi Wakurugenzi wamekuwa wakijificha kwenye revolving fund, wakitoa ile revolving fund ambayo imerudishwa na vikundi, utadhani ya kwamba imetolewa aislimia 10. Wizara mko tayari kuweka mchakato ambao utaweka wazi revolving fund na 10% ya mapato ya kila mwaka? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, naomba nikubali kwamba kwa maelekezo yako tutafanya hivyo ulivyosema kwa maana ya kupeleka nakala kwa kila Mbunge kueleza ufafanuzi tunamaanisha nini katika hii 10% ambayo inapaswa kuwa imetengwa.

Mheshimiwa Spika, lakini naomba nijibu sasa swali la nyongeza la Mheshimiwa Ryoba, ni kweli, wakati wa mjadala wa bajeti Waheshimiwa wa Kamati ya Utawala na TAMISEMI waliliona hili, na kweli imeonekana kuna halmashauri zingine wakichukua fedha wamekopesha, wakizirudisha, wengine walituambia ilionekana wanatoa taarifa ya kwamba walishapata mpaka asilimia 180, 120, wakaulizwa, hii nyingine ya ziada mmeitoa wapi. Ikaonekana kwamba, kikundi kikitoa fedha, wakikirudisha wanajumuisha wanasema imekusanywa, kwa hiyo, tukaelekeza kwamba na sasa hivi tumefungua akauti, kwenye kanuni mpya iliyotengenezwa, kutakuwa na akaunti mahususi ambayo fedha hii inaingia.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, umapokusanya fedha zitaonekana, zinaporejeshwa zitaonekana kwa hiyo, hakutakuwa na kuchanganya kati ya fedha ambayo imekopesha na fedha ambayo imekusanywa, lakini Waheshimiwa Wabunge kama nilivyosema, na hili nalo tutaona na nakala na kanuni watazipata ili kuweza kusimamia vizuri utengaji wa hizi fedha lakini usimamizi wake na utekelezaji wake.