Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 38 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 317 2019-05-29

Name

Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:-

Serikali imeziagiza halmashauri zote nchini kutenga asilimia tano ya vijana na asilimia tano ya wanawake kutoka mapato ya ndani ili kuchangia mfuko wa maendeleo wa wanawake na vijana:-

Je, Serikali inachukua hatua gani kwa halmashauri ambazo hazizingatii takwa hilo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMIESEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiteto Zawadi Koshuma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hapo awali utekelezaji na usimamizi wa mfuko wa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu, ulikuwa na changamoto kutokana na kutokuwepo kwa sheria na kanuni. Baadhi ya Halmashauri zimekuwa zikitenga asilimia 10 kutoka katika mapato yake ya ndani bila kujali vyanzo lindwa na fedha zenye maelekezo maalumu kama vile CHF na fedha zenye maelekezo maalumu.

Mheshimiwa Spika, mwezi Juni, 2018, Serikali ilifanya marekebisho ya Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa sura Na. 290 kwa kuongeza kifungu cha 37(a) ambacho kimeelekeza namna bora ya kusimamia fedha hizo. Kufuatia marekebisho ya sheria hiyo, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) imeandaa kanuni ambazo zimefafanua namna bora ya kutenga fedha hizo, kutoa mikopo na kusimamia utekelezaji wake. Kwa mujibu wa kanuni hizo, asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu itatengwa baada ya kutoa vyanzolindwa.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Ofisi ya Rais (TAMISEMI) itaendelea kuzismamia halmashauri kuhakikisha zinatekeleza sheria hii na kanuni zake za mfuko wa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu na hatua za kinidhamu na kisheria zitachukuliwa kwa halmashauri zitakazoshindwa kutekeleza sheria hiyo na kanuni zake. Ahsante.