Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA (K.n.y. MHE. RASHID A. SHANGAZI) aliuliza:- Mkoa wa Tanga ndiyo Mkoa wenye halmashauri nyingi zaidi kwa sasa ukiwa na jumla ya halmashauri kumi na moja:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuugawa mkoa huo ili kurahisisha shughuli za utawala na maendeleo?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nchi yetu kwa sasa ina miundombinu mizuri kuliko enzi za ukoloni au enzi zilizopita. Je, Serikali inaonaje kwa muda huu kupunguza idadi ya wilaya, idadi ya majimbo ya mikoa ili Serikali ipate pesa, i-save pesa kwa ajili ya kupunguza idadi ya mikoa, idadi ya majimbo na idadi ya wilaya?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, tumemsikia Mheshimiwa Ally Keissy kwa maoni yake na mtazamo wake lakini maeneo haya kiutawala yakiwepo majimbo ya uchaguzi ya Waheshimiwa Wabunge hawa wapendwa, wilaya, mikoa na maeneo mengine ya kata na vijiji yanaanzishwa kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa utakapofika wakati wa kuona kwamba kwa hilo wazo la Mheshimiwa Keissy ni muhimu kufanyiwa kazi tutalifanyia kazi. Kwa sasa msimamo ni kwamba tutaendelea kuimarisha maeneo yaliyopo kujenga miundombinu, kupeleka huduma mbalimbali za kijamii ili watu wote waweze kupata maisha ambayo ni bora zaidi.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA (K.n.y. MHE. RASHID A. SHANGAZI) aliuliza:- Mkoa wa Tanga ndiyo Mkoa wenye halmashauri nyingi zaidi kwa sasa ukiwa na jumla ya halmashauri kumi na moja:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuugawa mkoa huo ili kurahisisha shughuli za utawala na maendeleo?

Supplementary Question 2

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana ningependa kuuliza swali la nyongeza mji mdogo wa Mbalizi ulipewa mamlaka miaka 15 iliyopita na sasa hivi ina wakazi zaidi ya 100,000 na pia uwanja wa kimataifa wa Songwe uko katika eneo hilo. Sasa ni lini Mji mdogo wa Mbalizi utapewa hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji wa Mbalizi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi ni kwamba kwa sasa tunaendelea kuimarisha maeneo ya kiutawala yaliyoanzishwa. Wanapozungumzia kuanzisha halmashauri maana yake unaongezea miundombinu unahitaji huduma ya ukubwa zaidi na watendaji watakuwepo na majengo yataongezeka.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Mbunge aendelee kuvumilia tuimarishe kwanza hii miji midog iliyopo halmashauri zetu na katika nchi hii kuna mikoa mingi pia bado haina majengo ya kutosha ya kuwa mikoa na watendaji wengine. Tuna upungufu wa miundombinu katika halmashauri zetu pia Waheshimiwa Wabunge wenyewe bado wanadai ofisi za Wabunge hazijajengwa. Kwa hiyo, nadhani ukiangalia mahitaji yaliyopo na kuongeza eneo la utawala nadhani tupeane muda kidogo tutekeleze haya yaliyopo tukamilishe tutazingatia baadaye maoni yake, ahsante.

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA (K.n.y. MHE. RASHID A. SHANGAZI) aliuliza:- Mkoa wa Tanga ndiyo Mkoa wenye halmashauri nyingi zaidi kwa sasa ukiwa na jumla ya halmashauri kumi na moja:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuugawa mkoa huo ili kurahisisha shughuli za utawala na maendeleo?

Supplementary Question 3

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi kwa kiasi kikubwa swali langu linafanana na Mheshimiwa Njeza kumekuwepo confusion ya kuongeza maeneo na kupandisha hadhi. Mkoa wa Shinyanga tulishamaliza mchakato wa kupendekeza mji wa Kahama uwe manispaa na sifa zote tunakidhi na kigezo kikubwa kimekuwa ni suala la mapato ambayo halmashauri ya Manispaa ya Kahama ina uwezo wa kujiendesha kwa hiyo si changamoto kwa Serikali. Pia Mji wa Isaka na tulishafikisha wizarani je, ni lini Wizara kwa mtazamo maalum inaweza ikaruhusu Halmashauri ya Mji wa Isaka pamoja na Halmashauri ya Manispaa ya Kahama itaanza?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Naibu wangu kwa ufafanuzi mzuri sana. Katika swali hili lakini tunafahamu kwamba nishukuru Mheshimiwa Maige kwa concern yake; tuna maeneo makubwa matatu kwanza, kuna Halmashauri ya Mji wa Geita, Kahama, pamoja na Halmashauri ya Mji wa Kibaha ambao sasa iko katika suala la kufanya tathmini ya kuhakikisha kuzipandisha katika hadhi ya manispaa. Kwa hiyo lakini kuna utaratibu sasa hivi ambao tunaendelea kuufanya kwanza kutoanzisha maeneo mapya lakini hilo suala zima la hadhi tutalifanyia kazi pale jambo litakapoiva vizuri mtapata mrejesho Waheshimiwa Wabunge.