Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 35 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 287 2019-05-24

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA (K.n.y. MHE. RASHID A. SHANGAZI) aliuliza:-

Mkoa wa Tanga ndiyo Mkoa wenye halmashauri nyingi zaidi kwa sasa ukiwa na jumla ya halmashauri kumi na moja:-

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuugawa mkoa huo ili kurahisisha shughuli za utawala na maendeleo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi Mbunge wa Mlalo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua kuwa Mkoa wa Tanga ndio mkoa wenye halmashauri nyingi zaidi kwa sasa ukiwa na jumla ya halmashauri 11. Hata hivyo, kipaumbele cha Serikali kwa sasa ni kuimarisha maeneo ya utawala yaliyopo yaliyoanzishwa katika miaka ya hivi karibuni kwa miundombinu na huduma mbalimbali ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi kabla ya kuanzisha maeneo mengine mapya. Hivyo, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira wakati Serikali ikitekeleza azma ya kuimarisha maeneo yake yaliyopo ambayo yana upungufu wa miundombinu na huduma mbalimbali muhimu kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wetu.