Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA (K.n.y. MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI) aliuliza:- Ongezeko la tembo na wanyama waharibifu imekuwa kero kubwa sana kwa wananchi wanaoishi maeneo ya kando kando ya hifadhi na ziwa. Je, Seikali ina mkakati wa kudhibiti tatizo linalosabishwa na kadhia hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante pamoja na kadhia hiyo, Serikali imekuwa ikichukua muda mrefu sana kulipa fidia na kifuta machozi lakini gharama hiyo pia haiakisi gharama ya uharibifu unaofanywa.

Je, Serikali ipo tayari kubadili kanuni zake kwa kuongeza gharama za kifuta machozi?

Mheshimiwa Spika, binafsi nimekuwa nikichukua hatua ya kumpigia simu Meneja wa TAWA Maswa Game Reserve lakini amekuwa haonyeshi ushirikiano wowote.

Je, Serikali ipo tayari kuwapatia mizinga wananchi katika vikundi katika Kata ya Lukungu, Mwakiloba, Kilejeshi na Wilaya zote za Mkoa wa Simiyu ili kuweza kukabiliana na tatizo la tembo hao?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ni kweli yamekuwepo malalamiko ya muda mrefu ya kiwango kidogo cha kifuta machozi na kifuta jasho ambayo yamekuwa yakitolewa na Wizara yangu. Lakini nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara yangu inapitia upya viwango hivyo, na mara itakapokamilisha tutatangaza na kuwajulisha waathirika tumefanya marekebisho na nina imani ingawa haiwezi kulipa thamani halisi ya maisha ya mtu na mazao yaliyoharibika lakini itakuwa imeongeza kiwango ambacho tumekuwa tukitoa kwa sasa.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili nimefahamu kuwa Mheshimiwa Leah Komanya amekuwa akipiga simu mara kwa mara kutetea wananchi hasa wakati mazao yanapokuwa yamefamiwa na wanyama. Nimhakikishie tu kwamba huyu afisa ambaye hatoi ushirikiano tutampa maelekezo, lakini nitoe maelekezo kwa maafisa wetu nchi nzima kuhakikisha wana-respond haraka sana wanapopata taarifa za uwepo wa wanyama.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu sasa hivi wanyama hawa wameongezeka baada ya kudhibiti ujangili kwa kweli limekuwa ni tatizo lipo nchi zima. Kwa hiyo, niwaelekeze maafisa wanyamapori popote pale walipo kuhakikisha kwamba wana wajibika haraka wanapopata taarifa hizi ili kuweza kutoa ushirikiano kwa wananchi. Na nimhakikishi tutawasiliana ili tuweze kuona namna watakavyoweza kutoa mizinga hii ya nyuki katika maeneo ya vijiji hivi.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA (K.n.y. MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI) aliuliza:- Ongezeko la tembo na wanyama waharibifu imekuwa kero kubwa sana kwa wananchi wanaoishi maeneo ya kando kando ya hifadhi na ziwa. Je, Seikali ina mkakati wa kudhibiti tatizo linalosabishwa na kadhia hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuwa kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu katika Wilaya ya Arumeru katika kijiji cha Ngalinanyuki na hifadhi ya Taifa ya Mumera, na mpaka sasa hivi wananchi wale hawajafikia muafaka wa mgogoro huo.

Je, Serikali sasa ni wakati muafaka wa mimi na Mbunge aliyeapishwa leo na Mheshimiwa Waziri kuongozana mpaka Kijiji cha Ngalinanyuki kwenda kusikiliza wananchi wale ili kero yao ifikie muafaka?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri yaliyotolewa hapa Bungeni na Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kujibu swali na nyongeza na Mheshimiwa Catherine Valentine Magige kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwamba kwanza katika eneo la Arusha National Park ususani katika sehemu hiyo ya Momera hakuna mgogoro per se hakuna mgogoro unaoweza kuita mgogoro. Lakini kwa sababu wananchi walienda mahakamani na walishindwa, kwa hivyo eneo lote lile ambalo walikuwa wanalidai ni eneo la Serikali.

Mheshimiwa Spika, lakini pamoja na malalamiko ya wananchi na pamoja na kwamba wameshinda kesi mahakamani. Serikali imeona ikate sehemu ya eneo la Arusha National Park ambalo lilikuwa ni miongoni mwa mashamba yaliyokuwa ya settlers wa eneo lile ili kuwagaia wananchi waweze kuishi kwa raha na amani zaidi. Kwa hiyo, wakati process hiyo itakapokamilika wananchi wa Momera watapata eneo ambalo tunazungumzia.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuongozana nae kwenda kutoa maelezo hayo nitaomba aongozane na Mheshimiwa Naibu Waziri baada ya Bunge hili.

Name

Andrew John Chenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA (K.n.y. MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI) aliuliza:- Ongezeko la tembo na wanyama waharibifu imekuwa kero kubwa sana kwa wananchi wanaoishi maeneo ya kando kando ya hifadhi na ziwa. Je, Seikali ina mkakati wa kudhibiti tatizo linalosabishwa na kadhia hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. ANDREW J. CHENGE: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Wilaya Bariadi kama ilivyo wilaya ya Busega, Bunda na Serengeti ni miongoni mwa Wilaya au maeneo yanayopakana na Hifadhi ya Serengeti. Lakini kikosi dhidi ya ujangili ofisi zake zipo Bunda na ofisi hiyo ndio inahusika na malipo ya kifuta jasho na kifuta machozi. Imekuwa ni shida sana kwa wananchi wanaotoka nje ya eneo la Bunda kama Baridi na baya zaidi wanapokuja kufanya malipo haya wanakuja kulipia malipo haya kwenye guest house.

Je, ni lini Serikali itafungua ofisi ya KDU mjini Bariadi ili kuondokana na adha hii hasa kwa akina mama ambao hawapendi kwenda guest house kwenda kupokea malipo yao?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba ofisi yetu ya KDU kwa sasa kikosi cha ujangili ipo Bunda na ni kwa sababu tuliamini kwamba Bunda ni katikati na eneo la Serengeti. Lakini nimhakikishie kwamba eneo hili analo lizungumzia yeye la Bariadi linapakana na Maswa, tunao maafisa wetu wa wanyamapori na tunaye afisa wa wanyamapori katika Maswa Game Reserve na wengine.

Mheshimiwa Spika, tutakachofanya ni kuwaelekeza hawa watu wa KDU wahakikishe kwamba wanakuwa na mawasiliano ya haraka na watu wetu wa halmashauri ambao kwa utaratibu ni watu wa kwanza wanafika maeneo ambayo mazao yameharibiwa kabla ya maafisa wa KDU kufika ili kutupa taarifa na kuweza kurahisisha mfumo wa malipo. Kwa hiyo, tumechukua ushauri wake wa kuwa na ofisi Bariadi, na tutakapo liangalia suala hili kulingana na uwezo wetu tutalizingatia.