Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 33 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 276 2019-05-22

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA (K.n.y. MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI) aliuliza:-

Ongezeko la tembo na wanyama waharibifu imekuwa kero kubwa sana kwa wananchi wanaoishi maeneo ya kando kando ya hifadhi na ziwa.

Je, Seikali ina mkakati wa kudhibiti tatizo linalosabishwa na kadhia hiyo?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali Mheshmiwa Dkt. Raphael Masunga Chegeni Mbunge wa Busega kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kanuni za wanyamapori wakali na waharibifu za mwaka 2011 zimeanisha aina wanyamapori ambao wanapaswa kushughulikiwa kama wanyamapori wakali na waharibifu. Kwa mujibu wa kanuni hizo, jedwali la tatu limeorodhesha wanayapori hao ambao ni tembo, kiboko, mamba, nyati, chui na simba.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka mikakati ifuatayo katika kunusuru maisha na mali za wananchi kutokana na madhara yanayosababishwa na wanyamapori wakali na waharibifu:-

Mheshimiwa Spika, moja kufanya doria za udhibiti wa wanyamapori hatari na waharibifu, kupitia askari wa wanyamapori Tanzania, TAWA, Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Halmashauri za Wilaya na Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro na wadau wengine. Lengo ni kuhakikisha kwamba tukio lolote la uvamizi wa wanyamapori wakali na waharibifu linashughulikiwa kwa haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, mbili kutumia mbinu na teknojia mbalimbali mfano kupanda pilipili na kutundika mizinga ya nyuki pembezoni mwa mashamba, kufunga vitambaa vyenye vilainishi vya magari yaani oil kuzungushia mashambani na kutumia ndege zisizokuwa na rubani kwa ajili ya kudhibiti tembo.

Mheshimiwa Spika, tatu kuendelea kutoa elimu za uhifadhi kwa jamii ili wananchi waepuke kulima kwenye maeneo ya shoraba.

Mheshimiwa Spika, wapo wanyamapori waharibifu ambao wanaweza kushughulikiwa na mkulima mmoja mmoja pamoja na Wizara ya Kilimo. Wanyamapori hao ni pamoja na nyani, ngedere, tumbili, nguruwepori na ndege aina ya kwelea kwelea na wengine. Aidha, Wizara intoa rai kwa Maafisa Ugani wa kilimo kushirikikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii ili kutoa elimu kwa wananchi juu ya kukabiliana na changamoto zinazotokana na wanyamapori jamii.