Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Kupitia Sera ya Serikali ya kila kata kuwa na kituo kimoja cha afya, ni kata mbili tu zimebahatika kuwa na vituo vya afya kati ya kata kumi na saba (17) za Halmashauri ya Mji wa Mbulu; vituo hivi viko kwenye Tarafa za Daudi na Endagikot:- (a) Je, ni lini Serikali itajenga kituo kimoja cha afya Kata za Kainam au Muray kwa ajili ya kupeleka huduma ya afya katika Tarafa ya Nambis yenye kata nne na vijiji ishirini na mbili na wakazi 24,800 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012? (b) Serikali ina sera ya kutoa huduma za afya bila malipo kwa watoto walio chini ya miaka mitano na akina mama wajawazito; je, Serikali inachukua hatua gani katika vituo ambavyo bado vimeendelea kuchangisha kundi hili muhimu katika jamii?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa kazi kubwa iliyofanya ya ujenzi wa Vituo vya Afya vya Daudi na Tlawi. Hata hivyo, katika swali langu la msingi nilikuwa nimeomba kituo hiki kwa ajili ya tarafa kwa sababu Jimbo la Mbulu Mjini lina tarafa tatu, tarafa mbili zimeshapata vituo vya afya ambavyo ni vituo pekee katika Jimbo la Mbulu Mjini.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa Tarafa ya Nambis ambayo iko pembezoni kama sehemu ya vijijini haina kituo cha afya na ina zahanati mbili tu katika kata hizo nne. Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kutafuta fedha za dharura ili walau zahanati moja katika zile mbili kwenye tarafa hiyo ikapandishwa hadhi na kuongezewa majengo na miundombinu mingine ya huduma ili wananchi hao wapunguziwe adha ya kusafiri mbali na huduma bora zaidi za afya?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; katika mpango wa awali wa vituo viwili vya afya; Kituo cha Afya Tlawi na Kituo cha Afya Daudi, Serikali ilikuwa na nia njema ya kupeleka vifaatiba na vitendeakazi vya milioni 440. Je, ni lini sasa Serikali yetu itakamilisha upelekaji wa vifaa hivi vya milioni 440 katika Vituo vya Afya Daudi na Tlawi ili kuweza kuboresha huduma ya afya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, nikiri wazi kwamba Mheshimiwa Zacharia amekuwa ni mfuatiliaji sana na hata wiki iliyopita tulikuwa pamoja kujadili mambo mbalimbali katika jimbo lake.

Mheshimiwa Spika, saula la jinsi gani tupate fedha za haraka, naomba Mheshimiwa Mbunge nikuahidi kwa sababu kwanza ufahamu kwamba juzijuzi tulikuwa twende wote pamoja kule Jimboni Mbulu lakini kulikuwa na mkutano ule wa Ma-DC ambao ulikuwa unafanyika tumeshindwa kwenda. Kwa hiyo, ahadi yetu tunatarajia Mwezi wa Sita tutaenda hata ikiwezekana site hiyo tutaweza kufika. Lakini kikubwa zaidi tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo tutafute fedha kuisaidia hilo eneo ambalo umezungumza kwa lengo kubwa la kuwahudumia wananchi.

Mheshimiwa Spika, agenda ya vifaatiba ni kweli tumejenga vituo takribani 352 na katika vituo hivyo vituo 44 vya kwanza vimeshapata vifaa lakini vituo vingine bado vifaa vinakuja. Kwa hiyo, tutafanya kila liwezekanalo vituo vyote 352 ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambavyo Mheshimiwa Rais amevijenga vyote vitapata vifaa kwa lengo kubwa wananchi waweze kuhudumiwa vizuri. Kwa hiyo, usipate shida Mheshimiwa Issaay, tunalifanyia kazi.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Kupitia Sera ya Serikali ya kila kata kuwa na kituo kimoja cha afya, ni kata mbili tu zimebahatika kuwa na vituo vya afya kati ya kata kumi na saba (17) za Halmashauri ya Mji wa Mbulu; vituo hivi viko kwenye Tarafa za Daudi na Endagikot:- (a) Je, ni lini Serikali itajenga kituo kimoja cha afya Kata za Kainam au Muray kwa ajili ya kupeleka huduma ya afya katika Tarafa ya Nambis yenye kata nne na vijiji ishirini na mbili na wakazi 24,800 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012? (b) Serikali ina sera ya kutoa huduma za afya bila malipo kwa watoto walio chini ya miaka mitano na akina mama wajawazito; je, Serikali inachukua hatua gani katika vituo ambavyo bado vimeendelea kuchangisha kundi hili muhimu katika jamii?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la msingi lipo kwenye Jimbo la Mbulu Mjini na mimi nipo Jimbo la Mbulu Vijijini. Jimbo la Mbulu Vijijini kuna kata 18, Mheshimiwa Waziri umefika umekuta kituo kimoja cha afya kama mke wa Mkristo; unaonaje ndugu yangu? Maretadu wamejenga kituo cha afya wamefika lenta; utatupatia fedha ili walau tuwe na kituo cha pili cha afya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kweli nimefika Mbulu na ni kweli ni changamoto kubwa ndiyo maana Serikali katika eneo lile kutokana na shida kubwa tulianza na ujenzi wa Kituo cha Afya cha Dongobesh. Lakini hata hivyo tuliamua kutoa fedha zaidi ya shilingi 1.5 billion kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbulu Vijijini.

Mheshimiwa Spika, nafahamu Mbulu jinsi ilivyo kuna maeneo wengine wako katika Bonde la Ufa na wengine wako juu. Tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo kama maombi Mheshimiwa Mbunge alivyoyaacha mara kadhaa ofisini kwetu tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo wale watu wa kata zingine kule za mbali tuangalie jinsi gani tutafanya tupate fedha kuwasaidia ujenzi wa kituo cha afya.

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Kupitia Sera ya Serikali ya kila kata kuwa na kituo kimoja cha afya, ni kata mbili tu zimebahatika kuwa na vituo vya afya kati ya kata kumi na saba (17) za Halmashauri ya Mji wa Mbulu; vituo hivi viko kwenye Tarafa za Daudi na Endagikot:- (a) Je, ni lini Serikali itajenga kituo kimoja cha afya Kata za Kainam au Muray kwa ajili ya kupeleka huduma ya afya katika Tarafa ya Nambis yenye kata nne na vijiji ishirini na mbili na wakazi 24,800 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012? (b) Serikali ina sera ya kutoa huduma za afya bila malipo kwa watoto walio chini ya miaka mitano na akina mama wajawazito; je, Serikali inachukua hatua gani katika vituo ambavyo bado vimeendelea kuchangisha kundi hili muhimu katika jamii?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, Tarafa ya Bashnet iliyopo Babati Vijijini haina kituo cha afya hata kimoja na kilichopo kinatoa huduma sawasawa na zahanati. Je, ni lini Serikali itakumbuka Tarafa ya Bashnet? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, tunatambua changamoto ya Mkoa wa Manyara kwa ujumla wake na ndiyo maana Serikali tulitoa 3.9 billion kwa ajili ya vituo vya afya vile vyote na tumetoa takribani shilingi bilioni 3 kwa ajili ya hospitali za wilaya. Lakini hata hivyo, nafahamu Babati Vijijini ina changamoto kubwa ndiyo maana tulianza na Kituo cha Afya cha pale Magugu na kituo cha afya kingine, lakini mwaka huu tumewapatia ujenzi wa hospitali ya wilaya katika bajeti ya mwaka huu ambayo nimeisoma si muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, lakini eneo hilo Mheshimiwa Mahawe alilolizungumza tutalichukua kulifanyia kazi, nini kifanyike kwa haraka kwa mpango wa Serikali kuwahudumia wananchi wa Babati Vijijini, tunafahamu wengine wanatoka mbali na huduma hizi ni huduma za msingi kuokoa maisha ya akina mama wajawazito. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mahawe naomba ondoa hofu, kama upiganaji wako ulivyo wa kawaida kwa Mkoa mzima wa Manyara, kilio chako kimesikika tutakifanyia kazi.