Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. RHODA E. KUNCHELA aliuliza:- Sekta ya Madini inaongeza pato kubwa katika uchumi wa nchi. Je, Serikali iko tayari kutatua kero kwa wachimbaji wadogo na vibarua ambao wananyanyasika katika migodi mbalimbali hapa nchini?

Supplementary Question 1

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nina maswali mawili ya nyongeza, wachimbaji wadogo wadogo katika taifa hili wamekuwa ndiyo wagunduzi wa kwanza wa maeneo ya machimbo, hususan katika mikoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kutokana na ukiritimba unaoendelea kwa baadhi ya matajiri, especially katika Mkoa wa Katavi, wamekuwa wanapora maeneo ya wananchi baada ya kugundua kwamba kuna madini, wanawapora lakini wanakwenda kufanya mazingira ya rushwa kwenye ofisi za madini wanahakikisha wanapata leseni za uchimbaji na huku wakiwaacha wachimbaji hawa wakiendelea kutapatapa na kukosa maeneo ya kuweza kuchimba.

Nini sasa Serikali ifanye ili kuhakikisha inatatua janga hili ambalo linaleta umaskini mkubwa kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mkononi hapa nina malalamiko ya wachimbaji wadogowadogo ambao wameajiriwa sasa kwenye haya machimbo, wamekuwa wanasainishwa mikataba ambayo ni feki, wananyanyaswa na wanapokuwa wanadai mafao yao au wanadai mishahara yao wamekuwa wakifukuzwa na kupigwa, wengine na kufunguliwa mashitaka. Migodi hiyo iko katika Kata za Idindi, Isulamilomo, Magula, Kasakalawe pamoja na Society ambako ni katika Kata ya Magama.

Niambie Mheshimiwa Waziri ni lini utakuja sasa kuwasikiliza wachimbaji hao wadogo na kero na unyanyasaji ambao wanafanyiwa katika migodi hii ambayo nimeitaja?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimhakikishie, katika swali la pili kwamba niko tayari kuja Katavi, kuja kutembelea na kusikiliza kero za wachimbaji wadogo na tumekuwa tukifanya hivyo na nilikwenda Katavi, lakini vilevile niko tayari kwenda tena kama kweli kuna specific issue ambayo ninaweza kwenda kusikiliza na kuweza kuitatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile, labda nimweleza tu Mheshimiwa Mbunge, kwamba kama kuna matatizo ya waajiriwa, kwa sababu kwenye wachimbaji wadogo kuna waliojiajiri na walioajiriwa, kama kuna matatizo ya walioajiriwa na migodi, tunaomba hizo taarifa mtuletee. Yetote aliyeajiri na ananyanyasa wafanyakazi, sisi kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo inashughulika na masuala ya ajira ambao wanashikilia Sheria ya Kazi, tuko nao kushirikiana nao kuhakikisha kwamba tunatatua kero za wafanyakazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika swali lake la msingi Mheshimiwa Mbunge ameuliza katika masuala ya ushirika, ni kweli. Kuna vikundi vya ushirika, acha ushirika wa mazao, ushirika wa madini, tumewapa watu leseni mbalimbali kuchimba kwa ushirika, lakini unakuta wale wafanyakazi wanaochimba au wanachama wa vikundi vile, wananyanyaswa na viongozi wa vikundi hivyo. Tunaomba kutoa wito na tunatoa onyo, kwa wale ambao ni viongozi wa vikundi, wanawanyanyasa wenzao, waache mtindo huo mara moja kwa sabahu sasa hivi tunawashughulikia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hatusiti kuwanyang’anya leseni vikundi ambavyo havifanyo mikutano ya mwaka, havitoi taarifa ya mapato na matumizi, tuko tayari kuvifuta na kuwapa watu wengine kuchimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini, vilevile, katika alipozungumza Mheshimiwa Mbunge kwamba, wachimbaji wadogo ndiyo wagunduzi wakubwa wa machimbo. Nikubaliane na yeye, kuna baadhi ya maeneo wachimbaji wadogo kweli unakuta ndiyo wamevumbua wachimbaji na wamekuwa wakinyanyasika, sasa hivi mtindo huu tumeukomesha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile kuna maeneo mengine watafiti wanakuwa wanagundua, wanapofanya kazi zao wa utafiti, wachimbaji wadogo wanavamia maeneo yale, kwa sababu wanaona kwamba kuna hali na dalili ya uchimbaji. Kwa hiyo, kunakuwa ni maeneo ambayo unaweza kukuta wachimbaj wadogo wametangulia au watafiti wametangulia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Wizara ya Madini kwa kushirikiana na Tume ya Madini, tunayaangalia hayo na tunatatua kero mbalimbali zinazotokana na migogoro hiyo.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. RHODA E. KUNCHELA aliuliza:- Sekta ya Madini inaongeza pato kubwa katika uchumi wa nchi. Je, Serikali iko tayari kutatua kero kwa wachimbaji wadogo na vibarua ambao wananyanyasika katika migodi mbalimbali hapa nchini?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa kwenye migodi yetu kuna watu ambao wamejiajiri kwa ajili ya kugonga kokoto zile zinazodhaniwa zina dhahabu, vibarua hawa wamekuwa wakilazimishwa kununua vitambulisho vya ujasiriamali na jana kumetokea sintofahamu, kuhusu hao vibarua na Mtendaji wa Kata ya Nyugwa na kusababisha wale vibarua kuondoka kwenye maeneo yao ya kazi kwa kulazimishwa kununua vile vitambulisho.

Je, Waziri, uko tayari kumwambia Mtendaji huyo aahirishe hilo zoezi? Kwa sababu hawa wanajiajiri wao kwa kugongagonga kokoto kwa mchanga mchana kutwa shilingi 2000, leo unakwenda kumlazimisha mgongaji kokoto huyu kitambulisho cha elfu 20. Je, Waziri uko tayari kusitisha hilo zoezi?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna mgogoro mkubwa ambao pengine ni kutokutambua au kutokuelewa. Tunasema wajasiriamali, tamko la Mheshimiwa Rais amesema, wajasiriamali wote walipe elfu 20, ambao hawazidi shilingi milioni nne kwa mwaka, yaani mapato yao, hilo ni tamko na tayari kutekelezaji umeanza. Sasa katika masuala ya uchimbaji wa madini, kuna kodi za upande wa uchimbaji wa madini, ambazo kweli tunazitoza, mtu anapopata dhahabu kwa mfano, analipa asilimia sita mrabaha analipa asilimia moja kwa ajili ya clearance, hizo kodi zinaeleweka, lakini hao ni wachimbaji ambao tunawatambua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa wale wachimbaji wadogo, maeneo mengi, ma-DC wamekuwa wakienda kule na kuhakikisha kwamba, wale kwa sababu wanatambulika na wenyewe kama wajasiriamali, waliojiajiri. Nimshauri tu Mheshimiwa Mbunge, kwamba, ukichukua elfu 20, ukaigawanya kwa siku 365 ni shilingi 54 tu kwa siku, haiwezekani mtu anafanya biashara, asilipe chochote kabisa. Kwa sababu ile ile biashara ya mawe inaishia huko tu, tunayem-charge kodi kwenye upande wa migodi ni yule ambaye anapata dhahabu, hao wengine tunawapata vipi. Kwa hiyo, wapewe vile vitambulisho, kwanza tuwafahamu, lakini cha pili na wao wachangie kidogo pato la Taifa kwa kulipa shilingi 54 kwa siku, ambayo ni sawasawa na shilingi 20 kwa mwaka mzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RHODA E. KUNCHELA aliuliza:- Sekta ya Madini inaongeza pato kubwa katika uchumi wa nchi. Je, Serikali iko tayari kutatua kero kwa wachimbaji wadogo na vibarua ambao wananyanyasika katika migodi mbalimbali hapa nchini?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, Mji wa Tarime tuna Migodi midogo ya Buguti na Kibaga, tumekuwa tukishuhudia migogoro kwa wachimbaji wadogo kwenye mgodi wa Kibaga na Mgodi ule wa Kibaga leseni yake iko na Barrick kwa muda mrefu na nimeshawahi kuuliza hapa, Serikali ikasema kwamba ina- revoke leseni ya Barrick. Na kwa sababu leo Naibu Waziri imekiri kwamba zile leseni zote ambazo hazifanyiwi kazi mtaenda kuzifuta na kuwapa wachimbaji wadogo. Ningetaka kujua specifically, kwa wachimbaji wadogowadogo wale wa Kibaga, ni lini sasa ile leseni itaondolewa kwa Barrick ili waweze kupewa wachimbaji wadogowadogo wa Kibaga waweze kufanya kazi zao kwa ufasaha zaidi na bila kubughudhiwa?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tumekwishakutoa tamko, kwa leseni zote ambazo hazifanyiwi kazi, na hasa ambazo ziko kwenye utafiti na hazifanyiwi kazi, zirejeshwe, zirudishwe na sisi tuweze kutafuta namna ya kuwagawia wachimbaji wadogo na tunawagawia katika vikundi. Mheshimiwa Mbunge ameniuliza swali hilo lakini hakunipa specific namba ipi, naomba tu nilichukue suala hili, tuone ni leseni ipi, aidha ni ya uchimbaji, au ni leseni ya utafiti. Kama leseni ni ya utafiti na haifanyiwi kazi, sisi tutazirudisha, lakini nimhakikishie tu kwamba kuna leseni nne ambazo zilisharudishwa na watu wa Barrick maeneo hayo na wameshaturudishia sisi na walishaandika barua, tutaangalia namna ya kuangalia kuwagawia wachimbaji wadogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. RHODA E. KUNCHELA aliuliza:- Sekta ya Madini inaongeza pato kubwa katika uchumi wa nchi. Je, Serikali iko tayari kutatua kero kwa wachimbaji wadogo na vibarua ambao wananyanyasika katika migodi mbalimbali hapa nchini?

Supplementary Question 4

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, moja ya kero kubwa ya wachimbaji wadogo ilikuwa ni ile sheria ambayo tulipitisha hapa Bungeni, ya kodi ya zuio ya asilimia tano kwa bei ya kuuzia madini kwa wachimbaji wadogo, lakini Bunge lako tukufu mwaka huu mwezi wa pili tulibadilisha hiyo sheria na kuondoa hilo zuio.

Sasa nataka kujua utekelezaji baada ya kuondoa hiyo sheria umefikia wapi kwa sababu ile sheria ilikuwa inapelekea madini mengi kutoroshwa nje ya nchi? Ahsante sana.

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Silinde la nyongeza. Ni kweli kama alivyosema tumekuwa tukipata malalamiko ya baadhi ya watu, hasa maeneo ya Arusha na mikoa mingine kwamba, pamoja na kwamba withholding tax na VAT zimefutwa kwa mujibu wa sheria, wako watu wanaendelea kuzitoza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomab kutoa wito na kutoa maelekezo rasmi kwa watu wote wanaohusika kwenye utozaji wa kodi na tozo mbalimbali kwenye sekta ya madini. Kodi ambazo zimefutwa na Bunge hili hakuna mtu mwingine yeyote wa aina yoyote anaruhusiwa kutoza hizo kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ninasema hili na iwe marufuku kwa mtu yeyote na tutakapopata taarifa tena, kwa mtu ambaye anaendelea kutoza hizo kodi, hatua kali zitachukuliwa kwa mujibu wa sheria. (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. RHODA E. KUNCHELA aliuliza:- Sekta ya Madini inaongeza pato kubwa katika uchumi wa nchi. Je, Serikali iko tayari kutatua kero kwa wachimbaji wadogo na vibarua ambao wananyanyasika katika migodi mbalimbali hapa nchini?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona, ili niulize swali la nyongeza kuhusu madini. Sisi katika Wilaya ya Longido tuna madini ya aina ya Ruby, na kuna mgodi wa miaka mingi, unaoitwa Mundarara Ruby Mine na sasa hivi wachimbaji wadogowadogo wameibuka wametokeza baada ya kujua madini haya yana thamani na ninaamini Serikali itakuja kuwajengea uwezo.

Lakini swali langu ni kwamba, huu mgodi ambao ulianzishwa tangu kabla ya uhuru, ni wa nani, na kama ni wa Serikali, Serikali inafaidikaje na huu mgodi na ni asilimia ngapi kama kuna ownership ya joint venture na mwekezaji?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa, pale Mundarara, kuna mgodi ambao ni mgodi wa uchimbaji wa Ruby. Mgodi ule kabla, miaka ya 60, ni kwamba mgodi ule ulikuwa ni mali ya Serikali, na sisi tumeweza kufuatilia na tuliunda Tume ili kuona ni namna gani mgodi ule uliweza kuporwa. Nipende tu kusema kwamba tumelifuatilia na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mgodi ule unamilikiwa sehemu na Serikali na kuna kampuni nyingine ambayo ilikuwa inamiliki, lakini mgodi ule mpaka sasa hivi, asilimia 50 tunaumiliki sisi yaani Wizara ya Madini kupitia Shirika la Madini yaani la STAMICO.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, mgodi huu ulikuwa na mikiki mingi, ambako Tume tumeituma, tumetuma Tume ya watu maalumu, wafuatilie, watushauri tuone namna gani ya mgodi ule kuurudisha Serikalini au kutafuta namna ya kuweza kuungana na mchimbaji mwingine au mwekezaji mwingine na Serikali iweze kupata mapato yake kupitia shirika la madini la STAMICO.