Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 32 Energy and Minerals Wizara ya Madini 269 2019-05-21

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. RHODA E. KUNCHELA aliuliza:-

Sekta ya Madini inaongeza pato kubwa katika uchumi wa nchi.

Je, Serikali iko tayari kutatua kero kwa wachimbaji wadogo na vibarua ambao wananyanyasika katika migodi mbalimbali hapa nchini?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rhoda Edward Kunchela, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Wizara kupitia Tume ya Madini imeendelea kuweka mikakati ya kuwatambua wachimbaji wadogo kwa kuwapatia leseni za uchimbaji. Aidha, Wizara ya Madini imeendelea kuhamasisha watanzania kote nchini kujiunga latika vikundi kwa mujibu wa sheria ya vyama vya ushirika, ili waweze kupatiwa elimu kiurahisi kuhusu uchimbaji salama, utunzaji wa kumbukumbu na uzalishaji na namna ya kupata mikopo kwa riba nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wizara imedhamilia kuondoa kero za wachimbaji wadogo hasa za maeneo ya kuchimba ili kuwawezesha kujiajiri katika sekta ya madini. Aidha, nimeagiza Tume ya Madini kuhakikisha wamiliki wote wa leseni za utafiti ambazo hazifanyiwi kazi zifutwe ili maeneo hayo yamilikishwe wachimbaji wadogo wenye lengo la kuviendeleza ili kuongeza mchango kwa sekta ya madini katika pato la Taifa na kujenga uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, migodi yote hapa nchini, inaendeshwa kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na marekebisho yake ya Mwaka 2017 na kuzingatia kanuni za uchimbaji salama, mazingira na afya kwa wafanyakazi. Suala la unyanyasaji wa aina yoyote halikubaliki na mmiliki anayefanya hivyo atakuwa anavunja Sheria ya Madini na Sheria za Kazi Mahali pa Kazi. Aidha, natoa wito, kwa yeyote mwenye malalamiko ya msingi kutoa taarifa kupita ofisi za madini zilizoko mikoani mwao ili yaweze kushughulikiwa kwa mujibu wa sheria.