Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA (K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALOSS) aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua mgogoro wa muda mrefu kati ya kituo cha polisi Bububu na soko dogo la wananchi lililopo karibu na kituo hicho? (b) Je, kiutaratibu umbali kati ya kituo cha polisi na makazi ya wananchi ni hatua ngapi?

Supplementary Question 1

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kupata nafasi hii, nashukuru sana Mheshimiwa Waziri wa majibu yako mazuri lakini nitakuwa na suala moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa muingiliano umekuwa mkubwa na watu wamekuwa wengi, kwanini hiki kituo kisitafutiwe sehemu nyingine, kikajengwa huko, kikawa na nafasi kubwa kikaelekea kama kituo kweli cha polisi kuliko pale kilivyokaa, hakijapendeza wala haifai. Huku kituo, huku soko, nafikiri Serikali ifikirie kukihamisha kikapate nafasi kubwa zaidi na majengo ya kisasa yaliyokuwa bora zaidi. Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kuhusiana na hoja ya kuhamisha kituo hiki kwa sababu ya ufinyu wa nafasi kiusahihi ni kwamba eneo la kituo lile ni kubwa mno, labda Mheshimiwa Mbunge tukipata nafasi tukatembelee ili nimuoneshe. Ni juzi tu hapa kuna eneo ambalo liliwahi hata kupewa mwekezaji na kutokana na maelekezo ya Mheshimiwa Rais ya kwamba maeneo ya vyombo vya usalama yabakie kwa matumizi ya vyombo hivi tulitoa maelekezo na kuhakikisha kwamba tumemhamisha yule mwekezaji.

Mheshimiwa Spika, lakini utakumbuka pia hata eneo ambalo liko pembeni ya kituo cha polisi ambacho kimetumika kama soko kama alivyozungumza kwenye swali la msingi ni eneo pia la polisi ukiachia mbali eneo la nyuma ambalo ni kubwa. Kwa hiyo, kimsingi kuhamisha kituo hiki kwa sababu ya ufinyu wa eneo nadhani haitakuwa sahihi kwa sababu kuna eneo la kutosha. Cha msingi ni kuendelea kutoa wito kwa wananchi kutumia nafasi yao yoyote ya kuvamia maeneo ya polisi kuacha maeneo ya polisi yaendelee kutumika kwa ajili ya shughuli za kiusalama.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA (K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALOSS) aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua mgogoro wa muda mrefu kati ya kituo cha polisi Bububu na soko dogo la wananchi lililopo karibu na kituo hicho? (b) Je, kiutaratibu umbali kati ya kituo cha polisi na makazi ya wananchi ni hatua ngapi?

Supplementary Question 2

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri kwanza nikushukuru kwa kutupatia zile 150,000,000 ambazo zimetusaidia kujenga majengo ya polisi katika eneo la Bagara Ziwani na nyumba zinakamilika.

Mheshimiwa Spika, sasa eneo hilo halijawahi kufidiwa, wananchi hawajawahi kufidiwa tangu 2004, polisi wanajenga majengo yao, wananchi hawajalipwa fidia tangu 2004. Nini kauli ya Serikali juu ya wananchi hawa ambao wametoa eneo kwa polisi lakini hawajapatiwa fidia mpaka leo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa tunachukua pongezi kama Serikali kutokana na kazi ambayo inaendelea nchi nzima maeneo mbalimbali ya ujenzi wa nyumba za askari polisi.

Mheshimiwa Spika, la pili nimpongeze yeye binafsi kwa kufuatilia kwa karibu hii kadhia ya wananchi wake kutolipwa fidia. Hata hivyo, naomba nimhakikishie kwamba jambo hilo nimelichukua na tutalifanyia kazi na baadaye tutarudi kwake kuweza kumpatia majibu ya hatua ambazo zimefikiwa na changamoto gani kama zipo na nini mikakati ya Serikali katika kukabiliana na changamoto hizo ili hatimaye wananchi hawa waweze kupata fidia stahiki.