Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 31 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 252 2019-05-20

Name

Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA (K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALOSS) aliuliza:-

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua mgogoro wa muda mrefu kati ya kituo cha polisi Bububu na soko dogo la wananchi lililopo karibu na kituo hicho?

(b) Je, kiutaratibu umbali kati ya kituo cha polisi na makazi ya wananchi ni hatua ngapi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tauhida Cassian Galoss, Mbunge wa Viti Maalum lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, si kweli kuwa kuna mgogoro wa kiwanja kati ya wananchi na Jeshi la Polisi katika eneo la kituo cha polisi Bububu. Ndiyo sababu wakazi wa eneo hilo ikiwemo wafanyabiashara wa soko hilo dogo hupata huduma za kiusalama katika kituo cha Bububu bila shaka yeyote. Aidha, kiwanja kilipojengwa kituo cha polisi Bububu na majengo mengine ya kituo yanamilikiwa kihalali na Jeshi la Polisi ingawa kuna kibanda cha kuuza samaki karibu na kituo hicho cha polisi kinachoitwa soko dogo la wananchi. Kibanda hicho kipo kati ya kituo cha Polisi Bububu na majengo mengine ya kituo.

Mheshimiwa Spika, ni kweli upo utaratibu wa kuwepo kwa umbali kati vituo vya polisi, kambi za makazi ya askari ya wananchi. Hii ni kutokana na sababu za kiusalama kwa miundo mbinu ya Jeshi la Polisi. Aidha, kutokana na changamoto za makazi na ujenzi holela mijini. Uvamizi wa maeneo sehemu mbalimbali na kuongezeka kwa shughuli mbalimbali za kibinadamu zisizo rasmi imesababisha maeneo mengi ya vituo vya polisi kuingiliwa na kusogeleana na makazi ya wananchi.