Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. ALEX R. GASHAZA (k.n.y. MHE. OSCAR R. MUKASA) aliuliza:- Mwanzoni mwa mwaka 2016 wananchi wa Kijiji cha Kabukome Kata ya Nyarubungo Wilaya ya Biharamulo walivamiwa na tembo na kupoteza asilimia kubwa ya mazao yao:- Je, ni lini wananchi hao watapata fidia ya mazao yao?

Supplementary Question 1

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza. Kwa kuwa matukio haya yamekuwa yanajitokeza mara kwa mara hususan katika Kijiji hicho cha Kabukome; na kwa kuwa Serikali imetoa maelekezo kwa Halmashauri kwamba wananchi hawa waweze kuwasilisha madai yao ili waweze kulipwa kifuta jasho: Je, Naibu Waziri pengine baada ya Bunge hili kufika katika eneo hilo ili kuweza kushauriana pia na wananchi wa eneo hilo kuona ni namna gani ya kuweza kuzuia tukio hili lisiweze kuwa endelevu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa Kijiji hiki cha Kabukome kinavyoathirika inafanana sana na baadhi ya vijiji katika Jimbo la Ngara vinayopakana na Hifadhi ya Taifa ya Burigi - Chato, Kijiji cha Gwakalemela Kata ya Kasulu na Kijiji cha Rusumo Kata ya Rusumo kwa sababu matukio haya yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara, anaweza akafika pia katika maeneo hayo kwa ajili ya kushauriana na wananchi wanaoishi katika maeneo hayo namna gani ya kuweza kuendelea kudhibiti uvamizi wa wanyama hawa hasa tembo? (Makofi)

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba kumpongeza Mheshimiwa Alex Gashaza kwa kuwa mshiriki mzuri katika uhifadhi, amekuwa pia akitusaidia sana kurejesha mahusiano kati yetu na wananchi katika maeneo yanayozunguka pori la Burigi - Chato. Pia namshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Oscar Mukasa kwa sababu amekuwa akifuatilia sana haki za wananchi wake katika eneo hili ambalo wamepata mgogoro wa wanyama.

Mheshimiwa Spika, taratibu za kulipa fidia ndiyo zinazosumbua kwenye maeneo mengi. Inatakiwa mwananchi anapopata tatizo la kuliwa kwa mazao yake au kushambuliwa na wanyama, ndani ya siku tatu, kama ni shamba awe ametoa taarifa kwenye Serikali ya Kijiji; na Afisa wa Kilimo amekagua na kuwasilisha kwa Afisa Wanyamapori wa Wilaya. Afisa Wanyamapori au Afisa wa Kilimo wa Wilaya ndiye anayeleta taarifa hizi kwenye Wizara yetu nasi tunashughulikia.

Mheshimiwa Spika, kama ni shamblio la mauaji, Afisa wa Kijiji anatoa taarifa Polisi na Polisi na Daktari wanafanya postmortem na baadaye taarifa hizi zinafika kwenye Wizara yetu nasi tunaweza kulipa. Hata hivyo, sehemu nyingi taarifa hizi zinachelewa kufika, zinafanyika baada ya tukio kupita muda mrefu, kwa hiyo, wanapokwenda watu wa kufanya tathmini, wanakuta shamba lilishapata uoto mwingine wa asili.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi Wizara yetu iko tayari kutoa kifuta jasho na kifuta machozi mara tu tukio hili linaporipotiwa ndani ya muda.

Mheshimiwa Spika, swali la pili la Mheshimiwa Mbunge, anaomba mimi Waziri nipate nafasi kwenda Jimboni kuweza kushirikiana kutoa elimu katika vijiji vya Benako, Kalemela na Kasulo, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba niko tayari na nitafanya hivyo baada ya Bunge hili. (Makofi)

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALEX R. GASHAZA (k.n.y. MHE. OSCAR R. MUKASA) aliuliza:- Mwanzoni mwa mwaka 2016 wananchi wa Kijiji cha Kabukome Kata ya Nyarubungo Wilaya ya Biharamulo walivamiwa na tembo na kupoteza asilimia kubwa ya mazao yao:- Je, ni lini wananchi hao watapata fidia ya mazao yao?

Supplementary Question 2

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Wananchi wa vijiji vya Chemchemi, Tampori, Iyoli kule Kata ya Kingale pamoja na Muluwa Kata ya Serya wamekuwa wakipata athari kubwa sana kutokana na wanyama waharibifu hawa tembo, almaarufu kule Zanzibar, Unguja ya Kusini kama ndovu.

Mheshimiwa Spika, tunaishukuru sana Serikali, wameanza kufanya malipo ya vifuta jasho na vifuta machozi kuanzia mwaka 2016 kwa baadhi ya vijiji, lakini athari hizi zimeanza 2012, taratibu zote zilifuatwa na pia madai yakawasilishwa Wizarani.

Sasa Je, kuna mpango gani wa kufanya malipo ya maeneo yaliyoachwa tangu mwaka 2012 kwa watu wote na kwa maeneo yote ambayo yalipata athari?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sannda, Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba athari za wanyama zimeendelea kuwepo na kwa sasa hivi zimeendelea kusumbua nchi nzima. Labda tu nitumie nafasi hii kuwafahamisha Waheshimiwa Wabunge kwamba kabla ya miezi michache iliyopita, ilikuwa ni jukumu la TAWA peke yake kupitia kikosi cha KDU kwenda ku-respond na matukio ya wanyama waharibifu yanapotokea, lakini Wizara imefanya marekebisho kama ilivyo kwenye maelekezo na hivi sasa popote ambapo tuna Hifadhi ya Taifa au tuna pori la akiba iwe ni TANAPA au TAWA au ni TFS katika eneo hilo, wanawajibika ku-respond na wanyama waharibifu wanapotokea kwenye maeneo ya vijiji. Kwa hiyo, maelekezo haya tumeshayatoa kwenye Taasisi zetu zote hizi.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tulianza kulipa mwaka 2016 na hii ilisababishwa na kutokuwepo kwa kumbukumbu za kutosha huko nyuma. Mwaka 2018 peke yake Wizara yangu imelipa shilingi bilioni 1.6 kama kifuta jasho na fidia. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tatizo la kutokulipa huko nyuma pamoja na kumbukumbu lilikuwa pia ni tatizo la fedha.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, mwaka huu peke yake mpaka leo tuna madai ya wananchi yanayofikia takriban shilingi bilioni 3.2 lakini mfuko wetu hauwezi kuzidi shilingi bilioni 1.6. Kwa hiyo, pale ambapo kumbukumbu zitaonyesha kwamba kuna wananchi bado wanadai, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara yangu itafanya mpango wa kulipa.