Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO aliuliza:- (a) Je, ni nini sifa au vigezo vya kupata Halmashauri? (b) Inachukua miaka mingapi kuendelea kuitwa Halmashauri ya Mji Mdogo hadi kuwa Halmashauri kamili?

Supplementary Question 1

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, sasa naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Jimbo la Kilolo na Wilaya ya Kilolo ni kubwa sana na Mheshimiwa Waziri anajua; na kwa kuwa Halmashauri ya Mji Mdogo wa Kilolo ambayo ni Ilula ilianzishwa muda mrefu, zaidi ya miaka mitano, kwa kigezo kwamba ili kupunguza ukubwa wa wilaya na jimbo ili kuwafikia wananchi. Je, sasa haoni ni wakati muafaka sasa wa kuipa hadhi ya kuwa halmashauri kamili kwa sababu vigezo vyote vilivyotajwa hapa vimekamilika?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Wilaya ya Kilolo ina ukubwa na sifa zote zinazokubalika; na kwa kuwa vikao vingi vimeshakaliwa, je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kufika Wilaya ya Kilolo na kujionea mwenyewe jinsi mambo yalivyo tayari kwa kugawa kutupa halmashauri kamili?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya kaka yangu, Mheshimiwa Venance Mwamoto, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, suala la Mji wa Ilula nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge, ziara yetu ya kwanza ambayo nilifanya mimi na yeye ambayo impact yake ndiyo maana Kilolo leo hii imepatikana hospitali ya wilaya ya kisasa. Licha ya ziara ile, jambo lingine kubwa tulitembelea eneo la Ilula na maeneo mbalimbali na ni kweli; Halmashauri ya Kilolo ni kubwa sana maana inapatikana mpaka huku na Kibakwe, ukiangalia jiografia yake ni kubwa sana. Kwa hadhi ya eneo lile, hasa Ilula, inapaswa kuwa halmashauri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, maelekezo ya Serikali ya hivi sasa kwamba status quo inabakia kwamba mpaka pale Serikali ijipange kwa sababu maeneo yote sasa hivi yamesimamishwa kupandishwa hadhi, lakini japo kuwa hadhi inastahili lakini kwanza kipindi cha sasa itasubiri kwanza mpaka hizi halmashauri ambazo zimeshapandishwa tuweze kuziwekea infrastructure za kutosha.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo jambo hilo naomba nimwambie kwamba lipo katika pending issue pale ambapo sasa tukipewa go ahead na utaratibu utakapokwenda vizuri tutalifanyia kazi wala Mheshimiwa Venance Mwamoto asihofu.

Mheshimiwa Spika, ajenda ya ukubwa wa halmashauri yake kama nilivyosema awali mimi na yeye tumeshatembea sana mpaka katika yale madaraja yaliyokuwa hayapitiki. Nimhakikishie kwamba tumefanya kazi kubwa, Mheshimiwa Venance Mwamoto asihofu, pale muda utakaporuhusu jambo hilo Serikali italiangalia kwa jicho la karibu sana.