Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 59 2019-11-11

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO aliuliza:-

(a) Je, ni nini sifa au vigezo vya kupata Halmashauri?

(b) Inachukua miaka mingapi kuendelea kuitwa Halmashauri ya Mji Mdogo hadi kuwa Halmashauri kamili?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Venance Mwamoto, Mbunge wa Kilolo, Mkoani Iringa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya), Sura 287 na (Mamlaka za Miji) na Sheria ya Serikali za Mitaa Sura 288 zimeweka utaratibu wakuzingatiwa katika kupandisha hadhi maeneo ya utawala. Vigezo vya kuanzisha Mamlaka za Miji Midogo vimeainishwa kwenye Mwongozo wa Uanzishaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wa mwaka 2014, Kipengele Na.4.2.5 (a-q) na miongoni mwa vigezo muhimu ni pamoja eneo linalopendekezwa kuwa na idadi ya watu isiopungua 50,000, kata zisizopungua 3, vitongoji visivyopungua 30 na ukubwa usiopungua kilometa za mraba 150.

Mheshimiwa Spika, vigezo vya kuanzisha Halmashauri ya Wilaya au kuipandisha hadhi Mamlaka ya Mji Mdogo kuwa Halmashauri ya Wilaya vimeanishwa kwenye Kipengele Na. 4.2.4 (a-q) kama nilivyosema awali na miongoni mwa vigezo muhimu ni pamoja na uwezo wa kujitegemea kibajeti kwa walau 20% kutokana na mapato ya ndani, eneo lenye ukubwa usiopungua kilometa za mraba 5,000, kata zisizopungua 20, vijiji visivyopungua 75 na idadi ya watu wasiopungua 250,000. Hivyo, upandishaji wa hadhi wa Mamlaka za Mji Mdogo kuwa Halmashauri unategemea vigezo vilivyoainishwa na sio muda wa Halmashauri.