Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN aliuliza:- Utalii wa baharini (Diving unakua kwa kasi sana na hakuna chuo kinachotoa elimu hiyo hapa nchini:- Je, Serikali haioni kuwa tunapoteza ajira nyingi kwa vijana wetu?

Supplementary Question 1

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru nashukuru pia majibu ya Waziri kwamba amekiri kwamba Serikali haina Chuo inachotoa haya mafunzo, mafunzo yanayotoa ni ya swimming na snockling mafunzo haya ni muhimu sana kwa maisha ya watu wetu nchi yetu imezungukwa na bahari na maziwa na watanzania wengi wanatumia bahari na maziwa na mito kwa ajili ya kutafuta riziki zao.

Je, Serikali sasa haioni ni muda muafaka wa kuanzisha chuo na kama hawana walimu kutafuta walimu kuja kufundisha ili kuepusha maafa kama haya yaliyotokea Kilindini Kenya mtu amezama kwa siku saba hajatolewa katika bahari?

Swali la pili nchi yetu kama nilivyosema imezungukwa na bahari na mito na watu wetu asilimia kubwa ndiyo wanatumia bahari na mito kwa ajili ya kutafuta riziki zao.

Je, Serikali haioni sasa kwamba ni muda muafaka kutafuta vijana wakawafundisha risk who divers kwa ajili ya uokoaji zinapotokea ajali za baharini? Nakushukuru.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi ni kweli kwamba kama nchi hatuna chuo maalum kinachofundisha diving peke yake lakini vyuo vyetu vyote vya uvuvi ukianzia Nyegezi, Mbegani, Kunduchi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa wanafunzi wote wanaosoma masomo ya uvuvi au masomo ya sayansi ya majini lazima wasome somo hilo kama sehemu ya masomo ya lazima ya kufaulu na katika jibu langu la msingi nimesema kutokana na uhaba wa wataalamu Serikali ilikwisha chukua hatua ya kupeleka wataalamu watatu nje ya nchi ili wataalam hao watakaporejea waweze sasa kulichukulia somo hilo kama somo muhimu kwa ajili ya kwanza shughuli ya utalii lakini pili kwa ajili ya uokoaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba umefika wakati ambapo suala hili tunalichukulia kwa uzito mkubwa na mara wataalam hawa watakaporejea watatoa mafunzo kwa vijana wetu na kwa watu wote wanaoshughulika na kuongoza watalii.

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN aliuliza:- Utalii wa baharini (Diving unakua kwa kasi sana na hakuna chuo kinachotoa elimu hiyo hapa nchini:- Je, Serikali haioni kuwa tunapoteza ajira nyingi kwa vijana wetu?

Supplementary Question 2

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nilikuwa na swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri anakiri kwamba Kisiwa cha Mafia ni maarufu na ni eneo zuri sana kwa ajili ya snorkelling, scuba diving na aina nyingine za uzamiaji:-

Je, Serikali itakuwa tayari sasa kuleta hicho chuo ikakiweka Mafia ili wananchi wa Mafia wanufaike nacho? (Makofi)

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dau, Mbunge wa Mafia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye majibu ya nyongeza ya Mheshimiwa Yusuph; baada ya wataalam hao kurejea; na kwa sababu wataalam hao wametumwa na Serikali kwenda kuchukua masomo hayo maalum kupitia vyuo ambavyo vipo; ninachoweza kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge ni kwamba katika maeneo ambayo tutayapa kipaumbele ni pamoja na Kisiwa cha Mafia.