Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omary Ahmad Badwel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. OMARY A. BADWEL aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa baadhi ya wananchi wamekuwa wakinufaika na mradi wa TASAF ambao kwa kiasi umekuwa ukifanya vizuri, aidha mradi huu umefika vijiji vichache tu na vijiji vingine bado havijafikiwa na Serikali iliahidi kuwa vijiji vyote vitanufaika na mradi huu. (a) Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya mradi wa TASAF kufikia vijiji vyote nchi nzima? (b) Kumekuwa na utaratibu wa baadhi ya viongozi kukata fedha za walengwa wa TASAF moja kwa moja kwa kuwakatia bima, michango mbali mbali ya vijiji na kadhalika bila ridhaa yao. Je, Serikali inatoa kauli gani katika jambo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Pamoja namajibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri na ninampongeza kwa kazi nzuri, nilikuwa na maswali madogo mawili.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa katika miradi ya TASAF Awamu ya I na TASAF Awamu ya II, ulikowepo pia utekelezaji wa miradi ya miundombinu kama ujenzi wa barabara, ujenzi wa madarasa, miundombinu ya maji, utoaji wa fedha kwa ajili ya VIKOBA na miradi mingine mbalimbali, zikiwemo zahanati. Lakini baadaye katika TASAF three, TASAF Awamu ya II miradi hiyo kwa kiwango kikubwa iliondolewa, ama ilikuwepo kwa kiasi kidogo au haikuwepo kabisa.

Sasa je, katika huu mpango wa awamu ya pili wa TASAF inayofuata sasa miradi hii itahusika katika utekelezaji katika vijiji vyetua mbapo ilikuwa imetoa faida kubwa sana katika sekta mbalimbali? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili, kwa kuwa Awamu hii ya III ya ugawaji wa fedha kwa walengwa walikuwa wanakwenda kugawa fedha moja kwa moja kwa walengwa kwa maana hizi kaya maskini, lakini ilijitokeza pia uwepo wa kaya hewa, jambo ambalo lilisababisha fedha hizi za Serikali kwenda mahali ambapo kwa watu hawakuwa waaminifu na hivyo kutokufikia malengo yaliyokusudiwa.

Je, katika awamu hii ya pili ya ugawaji wa mradi huu wa fedha za TASAF Serikali imejipangaje kuhakikisha kwamba hakutokei tena walengwa hewa ili fedha hizi ambazo zimepangwa na Serikali kupelekwa huko ziweze kupelekwa huko ziweze kufanya kazi iliyokusudiwa?

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza na yeye ninampongeza akiwa mmoja wapo wa watu ma-champion mahiri katika kufuatilia walengwa wetu wa kaya maskini kupitia mpango wetu wa TASAF.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimjibu Mheshimiwa Mbunge kabisa kwamba, mpango wa kunusuru kaya maskini, ni kweli awamu ya kwanza ulihusisha sana miundombinu, na ninaomba niliambie Bunge lako Tukufu kwamba, katika awamu yetu hii ya tatu kipindi cha kwanza, ambacho kinaisha mwezi huu na kipindi cha pili ambacho kinaanza mwezi ujao wa 12 mwaka 2019, tutaendelea na mpango wa miundombinu lakini tutajikita zaidi katika public works, kwa maana ya kwamba, zile ajira kwa muda, kwa wale walengwa ambao wanatokana na kaya maskini sana ili waweze kufanya kazi, waweze kupata ujira na ajira katika kuwawezesha maisha yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la pili, anasema Serikali tumejipangaje katika awamu ya tatu, Awamu ya II niliambie Bunge lako Tukufu kwamba tumejipanga, Serikali ya awamu ya tano, kuhakikisha kwamba walengwa wote kuanzia sasa hivi tutakuwa tunawaendea kwa kutumia njia za kidijitali kwa maana ya GPS, tutakuwa tunapiga picha kwenye kaya husika, lakini tayari tumeshafanya pilot project areas katika Mtwara DC, katika Halmashauri ya Nanyamba, lakini hata kule Siha na changamoto tulizozipata kule, ndizo ambazo zitatufanya tuboreshe katika maeneo mengine ambayo tutafika katika sehemu yetu hii ya pili inayoanza mwezi ujao.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile naomba niliambie Bunge lako Tukufu kwamba pia tutakuwa tunawalipa walengwa kwa njia za kielektroniki, vilevile VIKOBA na tayari tumeshaweka mpango mkakati mwingine, kuhakikisha kwamba tutakuwa na wale wanaofuzu, kwa maana ya graduation, tutakuwa tunawapatia mafunzo na tunawaunganisha na taasisi za kifedha na hii yote ili kuweza kuwa na multiply effects. Ahsante.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMARY A. BADWEL aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa baadhi ya wananchi wamekuwa wakinufaika na mradi wa TASAF ambao kwa kiasi umekuwa ukifanya vizuri, aidha mradi huu umefika vijiji vichache tu na vijiji vingine bado havijafikiwa na Serikali iliahidi kuwa vijiji vyote vitanufaika na mradi huu. (a) Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya mradi wa TASAF kufikia vijiji vyote nchi nzima? (b) Kumekuwa na utaratibu wa baadhi ya viongozi kukata fedha za walengwa wa TASAF moja kwa moja kwa kuwakatia bima, michango mbali mbali ya vijiji na kadhalika bila ridhaa yao. Je, Serikali inatoa kauli gani katika jambo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa wanufaika wengi wa TASAF ni wazee wasiojiweza na wanatoka katika maeneo ya pembezoni na inapofikia siku ya kupokea mafao, huwa wanafika pale katika maeneo ya vijiji kwa kutumia usafiri na usafiri huo wanalipia zile fedha za mafao. Je, Serikali haioni umefikia wakati wa kubaini wazee hawa wasiojiweza na kuweza kuwapelekea zile fedha katika maeneo yao?

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, hapa wakati najibu maswali yangu ya msingi na ya nyongeza ya Mheshimiwa Badwel nimesema, mkakati mmoja wapo wa Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha tunaboresha, kwamba tutakuwa tunawalipa walengwa wote kwa njia za kielektroniki kwa maana ya kwamba tumegundua kwamba walengwa wengine walikuwa wanakatwa fedha zao bila ridhaa yao na wengine walikuwa wanadhurumiwa, ndiyo maana katika kuboresha, tumeamua kwamba tutakuwa tunawalipa kwa njia ya kielektroniki. Ahsante.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMARY A. BADWEL aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa baadhi ya wananchi wamekuwa wakinufaika na mradi wa TASAF ambao kwa kiasi umekuwa ukifanya vizuri, aidha mradi huu umefika vijiji vichache tu na vijiji vingine bado havijafikiwa na Serikali iliahidi kuwa vijiji vyote vitanufaika na mradi huu. (a) Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya mradi wa TASAF kufikia vijiji vyote nchi nzima? (b) Kumekuwa na utaratibu wa baadhi ya viongozi kukata fedha za walengwa wa TASAF moja kwa moja kwa kuwakatia bima, michango mbali mbali ya vijiji na kadhalika bila ridhaa yao. Je, Serikali inatoa kauli gani katika jambo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, kumekuwa na utaratibu mbovu kwa baadhi ya viongozi wanaogawa fedha hizi, wakitumia itikadi za kisiasa, ikiwepo ukiwa mwanachama wa chama fulani, unaweza ukapewa fedha hizo, lakini ukiwa mwanachama wa chama kingine hupewi fedha hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningeomba Serikali itoe tamko fedha hizi wanaotakiwa kupewa ni watu wa aina gani? (Makofi)

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli haina ubaguzi. Ni Serikali ya Watanzania wote. Naomba niliambie Bunge lako Tukufu kwamba pesa hizi zinazotokana na Mpango wetu wa TASAF ni kwa walengwa wote wanaotokana na zile kaya masikini sana na hakuna ubaguzi wowote. Nitoe rai na agizo kwamba yeyote atakayeleta ubaguzi katika kuhakikisha kwamba walengwa wanaotokana na mpango huu wa kunusuru kaya masikini wanasaidiwa, watoe taarifa na watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)