Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kutumia Kituo cha Forodha Manyovu ili kupitisha mizigo kwenda Burundi kwa kiwango cha kutosha?

Supplementary Question 1

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Naishukuru Serikali kwa majibu yao mazuri kabisa, sina wasiwasi na majibu kwani mmejibu vizuri kabisa.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa inavyoonekana future transport logistic kati ya Tanzania na Burundi itapitia Manyovu. Ameonesha kabisa kwamba Dar- es-Salaam – Kabanga ni kilometa 1330 na Dar-es-Salaam – Tabora – Manyovu ni 1273, kwa hiyo, katika mpango wetu wa Blueprint na Easy of Doing Business inaonesha kwamba siku za mbele wafanyabiashara watapitia Manyovu kupitia Tabora. Kwa kuwa iko hivyo, ni maandalizi gani sasa mmeyafanya kwa ajili ya kupokea biashara hiyo? Najua Serikali mtaendelea kujitahidi.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa, amesema kuna changamoto ya barabara kwa ajili ya kurahisisha biashara kwenda Burundi. Je, Wizara ya Ujenzi ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba hivi vipande vya barabara vinaisha haraka?

Name

Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kitu cha kwanza Mheshimiwa Obama anawatetea kweli ndugu zetu kule, napenda tu nimjulishe kwamba katika utaratibu wa ujenzi wa barabara ambayo inatoka Burundi - Manyovu – Kasulu - Nyakanazi, moja ya vipengele vya barabara ile baadhi ya huduma ambazo zitajengwa kwa fedha za Benki ya Maendeleo ya Afrika ni pamoja na kujenga Kituo cha Pamoja cha Forodha pale Manyovu ambacho kwa hakika itakuwa ni mkombozi wa kuharakisha biashara kati ya Tanzania na Burundi.

Mheshimiwa Spika, la pili, kwa upande wa Wizara ya Ujenzi pamoja na sisi kama Wizara ya Fedha karibu tumekamilisha jitihada za kupata fedha za kukamilisha vile vipande ambavyo vimebaki vya barabara ambayo inatoka Manyoni - Tabora - Kigoma. Fedha zimekwishapatikana, tunakamilisha taratibu za ujenzi kwa kushirikiana na wenzetu wa Wizara ya Ujenzi. Ahsante.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kutumia Kituo cha Forodha Manyovu ili kupitisha mizigo kwenda Burundi kwa kiwango cha kutosha?

Supplementary Question 2

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mbali na Kituo cha Kabanga, kuna Kituo kidogo cha Forodha cha Murusagamba ambacho kinalelewa na Kituo cha Kabanga. Je, Serikali ina mkakati gani wa kupandisha hadhi Kituo hiki cha Murusagamba ili kiweze kuwa kituo kamili hasa kwamba upo mkakati wa kuunganisha barabara ya lami kutoka Nyakahura – Murusagamba - Burundi route ambayo pia itaendelea kuwa karibu? (Kicheko)

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Ngara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa sasa hivi ina Vituo vya Forodha vipatavyo 97 na upandishwaji wa Vituo vya Forodha kutoka kuwa vituo vidogo kuwa vituo kamili vya forodha huwa vina criteria yake ambayo na Kituo cha Murusabanga nacho tutaendelea kukifanyia kazi na tathmini. Kikikidhi vigezo vya kupandishwa hadhi na kuwa kituo kamili cha forodha kutokana na shuguli nyingi za kiuchumi zinazofanyika maeneo yale, Serikali haina shaka kukipandisha kituo hicho na Mheshimiwa Mbunge wa Ngara tuko tayari kufika tuweze kufanya tathmini hiyo.