Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itawadhamini Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ili waweze kupata mikopo kama ilivyo kwa Madiwani na Wabunge? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho/mishahara Wenyeviti wa Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini ningependa kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ni kiongozi wa kwanza wa ngazi ya Mtaa, lakini ukiangalia kazi kubwa anayoifanya katika kusimamia majukumu mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuwanganisha wananchi kwenye Mtaa wake pamoja na kusimamia ulinzi na usalama kwenye Mtaa wake, kiwango cha posho wanazopewa na Halmashauri ni kidogo…

SPIKA: Sasa swali.

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, napenda kujua, ni lini sasa Serikali itaongeza kiwango hiki cha posho wanayopata ya shilingi 10,000/= kulingana na kazi ambayo wanaifanya?

Mheshimiwa Spika, swali la pili la nyongeza, napenda kujua kwamba Waheshimiwa Madiwani sasa wanadhaminiwa kukopeshwa mikopo kutoka kwenye vyombo vya fedha: Ni lini sasa Serikali itasimamia kuhakikisha kwamba Wenyeviti nao wanakopeshwa katika vyombo vya fedha? Ahsante sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, swali la kwanza anazungumzia kiwango cha posho kwa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa. Kama ambavyo nimejibu kwenye swali langu la msingi ni kwamba ni kweli kwamba Wenyeviti hawa wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa wanafanya kazi kubwa na Serikali inawadhamini.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, mapato ambayo wanapewa ya asilimia 20 ni makusanyo katika Halmashauri husika. Hivi viwango vya shilingi 10,000/=, shilingi 20,000/=, shilingi 50,000/= mpaka shilingi 100,000/= vinategemeana pia na uwezo wa Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine wote, kadri tunavyokuwa tunabuni vyanzo mbalimbali kwenye Halmashauri zetu, zikipata uwezo mkubwa Wenyeviti hawa watapata posho kulingana na mapato ya ndani kulingana na Sura ya 290 ya fedha za Serikali za Mitaa kama nilivyotaja.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, anauliza ni lini Wenyeviti wataanza kupata mikopo? Yeye mwenyewe Mheshimiwa Mbunge amesema hiki kiwango ni kidogo na wakati mwingine ni kweli kwamba Wenyeviti wa Mitaa wanaendelea kudai. Kwa hiyo, namna ya kurejesha ukikopeshwa fedha benki inakuwa na ugumu wake, inaonekana mapato pia hayana uhakika. Halmashauri wanaweza wakapata kiasi kidogo, wakapata kidogo. Wakati mwingine kulingana na msimu wakapata fedha nyingi, wakapata nyingi kidogo. Sasa mabenki yatakuwa ni ngumu sana kuweza kuwawezesha.

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuja na mpango wa kuwezesha Halmashauri kuwa na miradi ya kimkakati, Halmashauri ikiwa na uwezo mkubwa wa kutosha kuanzisha kama masoko, stendi na vitu vingine vile vikubwa itawawezesha Halmashauri kuwa na uwezo, kuwa na kipato cha uhakika na Wenyeviti wetu watakopeshwa na watasimamiwa na Halmashauri na Waheshimiwa Wabunge katika maeneo yao ya kazi. Ahsante.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itawadhamini Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ili waweze kupata mikopo kama ilivyo kwa Madiwani na Wabunge? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho/mishahara Wenyeviti wa Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili nami niulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mwaka 2000 mpaka 2010 Serikali iliunda Tume ya Kushughilikia maslahi ya Madiwani na tume hii iliongozwa nami na iliitwa Tume ya Lubeleje kwa ajili ya maslahi ya Madiwani, kwamba Madiwani waongezwe posho kulingana na majukumu yao:-

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri unasema nini kuhusu kuongeza posho ya Madiwani pamoja na kuwalipa Wenyeviti wa Vijiji na Mitaa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ni nia na lengo kubwa la Serikali ikiwa na uwezo mkubwa unaotosha tungependa kuongeza posho hii ya Waheshimiwa Madiwani ili waweze kujikimu kulingana na kazi wanazofanya katika Halmashauri zetu ambazo ni kubwa.

Mheshimiwa Spika, swali la msingi hapo mwenyewe umeshuhudia, Mheshimiwa Mbunge anauliza, ni lini Wenyeviti wa Mitaa na Vitongoji wataongezwa posho?

Mheshimiwa Spika, nchi hii tuna mitaa zaidi ya 4,200 na kitu hivi; tuna vijiji zaidi ya 12,000; tuna vitongoji zaidi ya 64,000; na kila mtaa una Wajumbe sita, Kijiji kina Wajumbe 25. Ukipiga hesabu kwa ujumla wake, ni watu wengi kwelikweli; ongeza Madiwani wa Kata na Madiwani wa Viti Maalum.

Mheshimiwa Spika, naomba Waheshimiwa Madiwani waendelee kuchapa kazi, Serikali ya CCM inawaheshimu sana. Uwezo ukipatikana watapata posho, lakini tumeelekeza Halmashauri, wale Madiwani ambao wanadai posho zao na kukopwa, wasikopwe, walipwe kile ambacho kinawezekana kupatikana ili wachape kazi yao. Nakushukuru sana.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itawadhamini Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ili waweze kupata mikopo kama ilivyo kwa Madiwani na Wabunge? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho/mishahara Wenyeviti wa Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 3

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa na Vijiji wamekuwa wakifanya kazi nzuri sana katika maeneo yetu lakini wengi wao hawana ofisi na wengineo wanatumia nyumba zao kama ofisi:-

Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba Wenyeviti wetu wanapata ofisi ili waweze kufanya kazi zao vizuri sana katika Halmashauri zetu?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nashukuru. Ni kweli kuna baadhi ya maeneo ambayo Wenyeviti wetu wa Vijiji na Mitaa hawana ofisi, lakini wengine wamepanga katika nyumba za watu binafsi na wakati mwingine wanalazimika kufanya kazi hizo za kuhudumia wananchi katika majengo yao binafsi. Maelekezo ya Serikali ni kwamba Wenyeviti wa Mitaa ofisi zao zinasimamiwa na Halmashauri na Wakurugenzi katika maeneo yao, kwa sababu Watendaji wa Mitaa na Vijiji ni Wawakilishi na wanafanya kazi kwa niaba ya Mkurugenzi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nielekeze Halmashauri zote, kwenye bajeti zao za kila mwaka lazima watenge bajeti ya kujenga ofisi hata kama siyo zote, ndiyo maelekezo. Nasi tunaendelea kufuatilia na tuna taarifa za Halmashauri kuna baadhi wameanza kujenga ofisi hizo kwa kupitia michango mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, nawapongeza Waheshimiwa Wabunge pia, nimeona kwenye taarifa kwamba kwenye Mfuko wa Jimbo baadhi ya Wabunge tena wengine wa Viti Maalum wamechangia ujenzi wa Ofisi za Mitaa na Vijiji, lakini kuweka zana kama photocopy machine na kusaidia utendaji uweze kuboreshwa.

Mheshimiwa Spika, tuwahimize Wakurugenzi kile kinachopatikana kila mwaka kwenye bajeti yao na Waheshimiwa Wabunge wafuatilie, tutenge kiasi kidogo ili kuweza kupunguza shida za Ofisi za Wenyeviti wetu wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji. Ahsante.