Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 2 2019-11-05

Name

Hassan Selemani Kaunje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:-

(a) Je, ni lini Serikali itawadhamini Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ili waweze kupata mikopo kama ilivyo kwa Madiwani na Wabunge?

(b) Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho/mishahara Wenyeviti wa Serikali za Mitaa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Seleman Kaunje, Mbunge wa Lindi Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inalipa posho ya Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani yanayorejeshwa na Halmashauri kwenye Vijiji na yanayokusanywa kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290. Madiwani, Wabunge hudhaminiwa kupata mikopo kwenye mabenki na taasisi za kifedha kupitia posho za kila mwezi ambacho ni kipato chenye uhakika kuwezesha kurejesha mikopo hiyo waliyokopa.

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali ni kuziwezesha Halmashauri kubuni vyanzo vipya vya mapato ili kuimarisha makusanyo ya ndani katika vyanzo mbalimbali na kuimarisha uwezo wa Halmashauri kulipa posho hizo kwa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa. Ahsante.