Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATEMBE aliuliza:- Mradi wa maji wa Kitinku/Lusilile ndiyo uliotarajiwa kuwa mkombozi wa Wananchi wa Manyoni katika kupata huduma ya maji safi na salama, lakini mradi huo kwa muda mrefu umekwama kutokana na fedha kutopelekwa:- Je, Serikali ina mikakati gani ya kukamilisha mradi huo muhimu kwa wakati ili kumtua ndoo kichwani Mwanamke wa Manyoni?

Supplementary Question 1

MHE. AYSHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Mradi wa Maji Kintinku Lusisile, ulianza kutekelezwa chini ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa mwaka 2012, lakini hadi sasa imepita miaka saba mradi huu haujakamilika. Je, Serikali inasema nini kutokukamilika kwa mradi huu kwa wakati?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa, mojawapo ya tatizo kubwa la kutokukamilika kwa mradi huu ni ucheleweshwaji wa malipo, mpaka sasa tumepokea shilingi milioni 750 nje ya shilingi bilioni 2.2 tangu kusainiwa kwa mkataba tarehe 23 Mei, 2018. Nataka commitment ya Serikali ni lini mradi huu utakamilika? Wananchi wa Jimbo la Manyoni Mashariki wameteseka kwa muda mrefu, Mheshimiwa Naibu Waziri naomba unipe majibu, nakushukuru.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, nitumie nafasi hii kwanza kumpongeza Mheshimiwa Mbunge, kiukweli ni miongoni mwa Wabunge ambao wamekuwa wakipigania hasa upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Singida. Na ninataka nimhakikishie moja ya changamoto kubwa sana tukiri ilikuwa ucheleweshaji wa kukamilika kwa miradi ya maji. Tunashukuru sana Bunge lako Tukufu kwa kutupa rungu la kuanzisha Wakala wa Maji Vijijini, hatuna sababu hata moja sisi kama viongozi wa Wizara ya maji. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Wizara tumejipanga vizuri na wakala huu wa maji umejipanga vizuri. Tutahakikisha mradi ule tunaukamilisha kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kikubwa utekelezaji wa miradi ya maji unategemeana na fedha. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mwezi huu tunawapa fedha, si yeye tu hapo Manyoni, na hata kwa Mheshimiwa Massare katika mradi wake ule wa Itigi ambao unatekelezwa na Nangai tutatoa fedha katika kuhakikisha miradi hii ya maji inakamilika kwa wakati na Wananchi wa Manyoni waweze kupata huduma ya maji. Pia, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Lubeleje, jana alizungumza hapa eneo la Bulima na Iyoma na Mima wote nao tutaweza kuwapatia huduma ya maji, ahsante sana.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATEMBE aliuliza:- Mradi wa maji wa Kitinku/Lusilile ndiyo uliotarajiwa kuwa mkombozi wa Wananchi wa Manyoni katika kupata huduma ya maji safi na salama, lakini mradi huo kwa muda mrefu umekwama kutokana na fedha kutopelekwa:- Je, Serikali ina mikakati gani ya kukamilisha mradi huo muhimu kwa wakati ili kumtua ndoo kichwani Mwanamke wa Manyoni?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, asante kwa nafasi hii, katika Halmashauri ya Lushoto, Kata ya Manolo kuna mradi ambao umesainiwa tangu mwaka 2013, tunavyozungumza hadi sasa Serikali imeshalipa hela zote kwa mkandarasi, lakini jambo dogo la shilingi milioni 82 za VAT Serikali imeshindwa kuondoa na mpaka sasa hivi wananchi wale wanapata shida tangu mwezi wa sita mpaka sasa hivi shilingi milioni 82 imekuwa ni kikwazo cha Wananchi wa Manolo kupata maji safi na salama.

Je, Serikali inatoa kauli gani kwa Wananchi hawa wa Manolo ambao wanaendelea kuteseka kwa kukosa maji safi na salama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge. Kiukweli Mheshimiwa Shangazi mradi huu umeupigania sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya changamoto ilikuwa ni suala la fedha, mkandarasi alikuwa akidai takribani milioni 600 na sisi kama Wizara ya maji tulitengeneza commitment na tukamlipa ile fedha. Sasa hii changamoto ya VAT nataka nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge Serikali haijawahi kushindwa, sisi kama Wizara ya Maji tupo tayari tutakaa na Wizara ya Fedha haraka katika kuhakikisha changamoto hii tunaitatua kwa haraka, ili Wananchi wako waweze kupata huduma ya maji safi na salama, ahsante sana.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATEMBE aliuliza:- Mradi wa maji wa Kitinku/Lusilile ndiyo uliotarajiwa kuwa mkombozi wa Wananchi wa Manyoni katika kupata huduma ya maji safi na salama, lakini mradi huo kwa muda mrefu umekwama kutokana na fedha kutopelekwa:- Je, Serikali ina mikakati gani ya kukamilisha mradi huo muhimu kwa wakati ili kumtua ndoo kichwani Mwanamke wa Manyoni?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii:-

Mheshimiwa Naibu Spika naishukuru sana Serikali nilishawahi kuongea na Mheshimiwa Waziri kuhusu tatizo la maji katika Kata ya Magadu, wananchi wanapata matatizo kwa muda mrefu. Na chanzo cha maji kutokana na utafiti ni kuwa tayari kilishapatikana kutoa mbete. Je, kuna tatizo gani la kuendeleza hicho chanzo cha maji kuhusu Wananchi wa Magadu na mitaa mingine waweze kupata maji ya kutosha?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, kiukweli nimpongeze Mheshimiwa Mbunge amekuwa mfuatiliaji sana na ameshafanya kikao na Mheshimiwa Waziri. Nataka nimuombe basi baada ya Bunge tukutane na wataalam wetu tuangalie namna gani ya kuweza kuwasaidia Wananchi wa Magadu.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATEMBE aliuliza:- Mradi wa maji wa Kitinku/Lusilile ndiyo uliotarajiwa kuwa mkombozi wa Wananchi wa Manyoni katika kupata huduma ya maji safi na salama, lakini mradi huo kwa muda mrefu umekwama kutokana na fedha kutopelekwa:- Je, Serikali ina mikakati gani ya kukamilisha mradi huo muhimu kwa wakati ili kumtua ndoo kichwani Mwanamke wa Manyoni?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, kwanza napenda kumshukuru Naibu Waziri maana tarehe 07 Agosti, alikuja Wilaya ya Tarime na kuna maagizo aliyatoa kwenye Mradi wa Gamasara na wa Nyanduluma, lakini nataka kujua ni lini sasa vile visima 23 ambavyo Bunge lililopita niliuliza hapa na ukaelekeza kwamba, ni DCA wanaenda kuanza kuvichimba mara moja, lakini mpaka sasa hivi hamna chochote ambacho kinaendelea kwenye Jimbo la Tarime Mjini, ili kuweza kutoa suluhisho la la muda mfupi wakati tukisubiri ule mradi wa Ziwa Viktoria? Ahsante?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, nikiri nimefika Tarime na moja ya changamoto kubwa kiukweli changamoto kubwa ipo pale Tarime. Na moja ya changamoto ambayo tumeona jambo la kulifanya haraka kwanza tume-terminate mkataba wa yule mkandarasi wa Mradi wa Gamasara, mradi ule tutaufanya kwa sisi wenyewe kuwapatia fedha wataalam wetu waweze kuutekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia kuna suala la uchimbaji wa visima. Tumekwishawaagiza watu wa DDCA na sisi tumejipanga kuwapatia fedha ili uchimbaji wa visima 23 uweze kuchimbwa pale wakati tunasubiri mradi mkubwa wa fedha zile za India. Sisi kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo kwa wananchi wa Tarime kupata huduma ya maji safi na salama.