Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 27 2019-09-04

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATEMBE aliuliza:-

Mradi wa maji wa Kitinku/Lusilile ndiyo uliotarajiwa kuwa mkombozi wa Wananchi wa Manyoni katika kupata huduma ya maji safi na salama, lakini mradi huo kwa muda mrefu umekwama kutokana na fedha kutopelekwa:-

Je, Serikali ina mikakati gani ya kukamilisha mradi huo muhimu kwa wakati ili kumtua ndoo kichwani Mwanamke wa Manyoni?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aysharose Ndogholi Matembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji Kintinku Lusilile ulibuniwa kwa lengo la kuhudumia vijiji 11 vyenye wakazi wapatao 55,485 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012. Vijiji hivyo ni Kintinku, Lusilile, Maweni, Mvumi, Ngaiti, Chikuyu, Mwiboo, Mbwasa, Mtiwe, Makutupora na Chilejoho. Kwa mujibu wa usanifu uliofanyika mradi huu unakadiriwa kugharimu bilioni 10.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa mradi huu umepangwa skutekelezwa katika awamu nne ambapo awamu ya kwanza ilihusisha utafiti na uchimbaji wa visima vinne na utekelezaji wake ulikamilika. Hivi sasa utekelezaji wa awamu ya pili unaendelea ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni tarehe 23 Mei, 2018 iliingia mkataba na Mkandarasi CMG Construction Company Limited kutekeleza awamu ya pili ya mradi huo ambao ulitarajiwa kukamilika mwezi Novemba, 2018. Hata hivyo kutokana na changamoto ya upatikanaji wa fedha awamu hiyo haukuweza kukamilika kama ilivyopangwa na kwa sasa utekelezaji wa awamu ya pili umepangwa kukamilika mwezi Septemba 2019.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mikakati ya kuhakikisha tunaongeza kiwango cha upatikanaji wa maji katika Wilaya ya Manyoni, Wizara imetenga kiasi cha shilingi bilioni 2.4 kwenye mwaka wa fedha 2019/2020 kutekeleza miradi mbalimbali ya maji wilayani humo. Tayari RUWASA wamewasilisha maombi ya kuanza kutekeleza awamu ya tatu ya Mradi wa Maji wa Kintinku/Lusilile.