Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO aliuliza:- Katika viwango vya kidunia vya umeme vile ambavyo tunavyofuata, kuna mabadiliko ya rangi za nyaya za umeme yaliyotokea tangu mwaka 2004 kwa nchi yetu ya Tanzania:- Je, mabadiliko hayo yanafahamika kila mahali?

Supplementary Question 1

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza kabisa niishukuru Wizara kwa majibu yao mazuri lakini kiukweli mabadiliko hayajaanza kufundishwa vyuoni wala shuleni na TANESCO wamekuwa wakitumia nyaya za zamani. Kwa hiyo basi, kuna mkanganyiko mkubwa zaidi na ukizingatia sasa hivi tuko katika uchumi wa viwanda. Hivyo basi, naiomba Serikali yangu itafute namna sahihi ya kutatua mkanganyiko huu ili kuepusha athari zinazoweza kujitokeza katika kuchanganya nyaya za umeme. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, pamoja na kupokea ushauri kwa sababu jambo hili ni la muhimu, naomba nitoe maelezo kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, kimsingi hizi rangi hazina athari kwa ujumla wake isipokuwa chimbuko la mabadiliko haya ya rangi ilikuwa ni kwa ajili ya kuweka mazingira wezeshi kwa upande wa wenzetu ambao tumekuwa tukichukua standard zao (Commonwealth) walipokuwa wameungana na hawa nchi za Ulaya. Kwa hiyo, unakuta watu wa AU walikuwa na standard zao na watu wa British walikuwa na standard zao ilibidi wawianishe na ndiyo zikatokea hizi rangi nyingine ambazo zimejitokeza.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa mazoea, watu wetu walikuwa wamezoea mtindo huu wa red yellow, blue. Sasa kinachofanyika ni kwamba kupitia TBS, kuanzia mwaka 2010 tulianza kufanya huo uwianisho na tayari tumeshafikia hatua nzuri. Vilevile ili kuondoa hizi changamoto ambazo zinaweza kusababisha madhara kutokana na watu kuchanganya hizo rangi japo pia tunasisitiza na sheria inasema kwamba mtu anayefanya wiring installation iwe kwenye high voltage au low voltage lazima awe na uwezo wa kutosha na awe amethibitishwa au kama akifanya mtu mwingine asiyethibitishwa lazima apeleke kwa aliyethibitishwa.

Kwa hiyo, tunategemea kwamba TBS itakuja na huo mwongozo maalum unaoelekeza hizi standards ili sasa ziweze kutumika kwa mkazo zaidi. Hata hivyo, suala la mpito hilo hata kwenye nchi nyingine lilifanyika.

Mheshimiwa Spika, pia nawaomba wakandarasi wanapokuwa wamefanya kazi inayochanganya mfumo wa zamani na mfumo wa sasa, waweke maelekezo pale kwenye main switch ili mtu yeyote anayefika aweze kujua kwamba mfumo huu umechanganywa.