Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 59 2020-02-03

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO aliuliza:-

Katika viwango vya kidunia vya umeme vile ambavyo tunavyofuata, kuna mabadiliko ya rangi za nyaya za umeme yaliyotokea tangu mwaka 2004 kwa nchi yetu ya Tanzania:-

Je, mabadiliko hayo yanafahamika kila mahali?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA (K.n.y. WAZIRI WA NISHATI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Halima Abdallah Bulembo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mabadiliko ya rangi za nyaya za umeme ni jambo la kawaida katika taaluma ya uhandisi wa umeme, hivyo mitaala yote ya mafunzo ya uhandisi wa umeme yanazingatia mabadiliko haya. Mabadiliko ya rangi za nyaya za umeme yalitokea mwaka 2004 na hivi sasa yanafundishwa nchini kupitia Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA), Vyuo vya Ufundi Mchundo na Vyuo Vikuu. Aidha, somo la rangi za nyaya za umeme linafundishwa katika somo la Fizikia katika shule za Sekondari.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa umeme mkubwa kimazoea (high voltage) unakuwa na rangi tatu ambazo ni nyekundu, njano na bluu. Nyaya za rangi hizo huwa ni moto. Vilevile kwa umeme mdogo (low voltage) unaotumia njia tatu (three phase) unakuwa na rangi nne ambazo ni nyekundu, njano, bluu na nyeusi. Kwa upande wa umeme wa njia moja (single phase) unakuwa na rangi mbili nyekundu na nyeusi.

Mheshimiwa Spika, kutokana na mabadiliko hayo yaliyoanza mwaka 2004 na kukamilishwa mwaka 2006 ya BS 7671 (British Standard) iliyowianishwa rangi mpya kwa umeme mkubwa (High Voltage) ni kahawia, nyeusi na kijivu kwa umeme mdogo (low voltage) three phase, rangi mpya ni kijani yenye mchanganyiko na njano, bluu kwa nyaya za moto ni kahawia nyeusi na kijivu. Kwa upande wa njia moja (single phase) unakuwa na rangi mbili za kahawia na bluu. Serikali itaendelea kutoa elimu kwa watu wote wanaohusika na matumizi ya rangi hizi ikiwemo wakandarasi, wafanyabiashara, wenye viwanda na wananchi kwa ujumla.