Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati gereza la Keko ambalo miundo mbinu yake imechakaa sana?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, swali hili naliuliza kwa mara ya pili, niliuliza kwa mara kwanza kwama 2016 na Serikali kweli ni sikivu ilifanya ukarabati mdogo mwaka 2016/2017. Hata hivyo, ukarabati huo haukumaliza tatizo kwa sababu bado maji taka yanachirizika kutoka gerezani kwenda kwenye makazi ya watu na ni hatari zaidi kwa kipindi hiki cha mvua ambayo maeneo hayo mengi yamefurika na maji ya mvua. Kwa hiyo kuna hatari kubwa ya kutokeza magonjwa ya mlipuko.

Je, Serikali ipo tayari sasa kama hatuwezi kujenga mashimo ya kutosha basi tuzibe zile njia zisitiririshe maji kwenda kwenye makazi ya wananchi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, gereza hili ni gereza VIP ni gereza ambalo limejengwa kwa upekee sana ukifananisha na magereza mengine, ndio maana huhifadhiwa watu maarufu au wenye kesi kubwa kubwa, je, Serikali haioni kuna haja sasa ya kulitazama gereza hili kwa jicho lingine ili watenge fedha za kutosha kwa ajili ya kufanya ukarabati wa gereza lote kwa pamoja?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mtolea, Mbunge wa Temeke, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze wakati ule alivyoleta hoja yake ya changamoto ya gereza hili na yeye ameona uungwana wa kuipongeza Serikali kwa kutilia maanani yale aliyoeleza hapa Bungeni na tukayafanyia kazi. Nimhakikishie kwamba kama ambavyo tumefanya kipindi kile na haya ambayo ameyazungumza sasa hivi na yenyewe tatayachukua ili tuweze kuyafanyia kazi.