Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 26 2020-01-29

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati gereza la Keko ambalo miundo mbinu yake imechakaa sana?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Ally Mtolea, Mbunge Wa Temeke, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Gereza la Keko ni moja ya magereza yaliyojengwa wakati wa mkoloni, hivyo hata miundombinu yake imekuwa ni ya muda mrefu inayohitaji ukarabati. Hata hivyo, Serikali imekuwa ikifanya jitahada za ukarabati kulingana na fedha inavyopatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha katika mwaka wa fedha 2016/2017, Serikali ilifanya ukarabati wa mfumo wa maji taka kwa kuchimba mashimo ya kuhifadhia majitaka baada ya mashimo yaliyokuwepo kuzidiwa kutokana na idadi kubwa ya wahalifu waliomo ndani ya gereza hilo.