Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. RICHARD M. NDASSA (K.n.y. MHE. KISWAGA B. DESTERY) aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutumia mtandao wa maji Magu kupeleka Tarafa ya Ndagalu, Kata za Shishani, Njinjinili, Kabila, Nkungulu, Ng’haya, Sukuma, Buhumbi na Mwamabanza zenye jumla ya vijiji 24?

Supplementary Question 1

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niishukuru sana Serikali kwa majibu yake mazuri hasa kukamilisha angalau kupeleka maji katika Wilaya ya Magu pale Magu Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu; kwa sababu muuliza swali la msingi amezungumzia vijiji kadhaa ikiwemo pamoja na Kijiji cha Kabila ambacho kina wakazi wengi sana. Ili kuondoa tatizo la ukosefu wa maji na Mheshimiwa Waziri anajua kabisa kwamba maji ni uhai, ni lini sasa angalau kwa kuanzia kabla ya Mradi mkubwa huu wa Maji ya Ziwa Victoria haujaanza angalau kwenda kufufua vile visima ambavyo vilikuwepo kama ambavyo tunavyofanya sasa kwenye eneo la Jimbo la Sumve pamoja na Magu, lakini pia kusafisha vile visima ambavyo vilikuwa vinafanya kazi. Sasa Serikali kwa nini sasa isifanye utaratibu wa kuchimba na kusafisha vile visima ambavyo vilikuwepo? Nakushukuru.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ndassa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Mzee wangu, Mzee Ndassa sisi kama viongozi wa Wizara ya Maji tumeainisha Mikoa zaidi ya 17 yenye changamoto ya maji ikiwemo eneo la Mkoa wa Mwanza, lakini tumepata fedha kutokea World Bank na katika Mikoa hii 17 tumepeleka kila Halmashauri 1.3 billion ikiwemo katika Jimbo lake la Sumve.

Nimwombe sana Mhandisi wa maji akae na Mheshimiwa Mbunge na mimi mwenyewe nipo tayari ili katika kuhakikisha fedha zile zinaelekezwa katika zile changamoto ambazo Mheshimiwa Mbunge amezianisha. Ahsante sana.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. RICHARD M. NDASSA (K.n.y. MHE. KISWAGA B. DESTERY) aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutumia mtandao wa maji Magu kupeleka Tarafa ya Ndagalu, Kata za Shishani, Njinjinili, Kabila, Nkungulu, Ng’haya, Sukuma, Buhumbi na Mwamabanza zenye jumla ya vijiji 24?

Supplementary Question 2

MHE. BONIFACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Katika Jimbo la Bunda Vijijini kuna Mradi wa Maji Nyamuswa na kuna Mradi wa Maji Mgeta na Naibu Waziri ailifika kwenye maeneo hayo lakini mpaka sasa ile Kamati aliyoiunda kufuatilia shughuli hizo haijakwenda vizuri.

Je, Naibu Waziri yuko tayari sasa kushughulika na hilo jambo ili watu wa Nyamuswa na Mradi wa Mgeta-Nyangarangu wapate maji?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nipo tayari. Ahsante sana.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. RICHARD M. NDASSA (K.n.y. MHE. KISWAGA B. DESTERY) aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutumia mtandao wa maji Magu kupeleka Tarafa ya Ndagalu, Kata za Shishani, Njinjinili, Kabila, Nkungulu, Ng’haya, Sukuma, Buhumbi na Mwamabanza zenye jumla ya vijiji 24?

Supplementary Question 3

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Pamoja na shukurani za wananchi wa Jimbo la Mtama kwa miradi kadhaa inayoendelea ya maji katika Jimbo hilo baada ya Mji wa Mtama kupewa hadhi sasa ya kuwa Halmashauri mahitaji ya maji yameongezeka sana katika Mji huu. Je, Serikali sasa iko tayari kwenye bajeti ya mwaka huu kutenga fedha kwa ajili ya kuboresha miundombinu na upatikanaji wa maji katika Mji huu?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, Kaka yangu Mheshimiwa Nape.

Mheshimiwa Nape anafanya kazi kubwa na nzuri na alishakuja katika Ofisi yetu ya Wizara ya Maji, tukakaa mimi, yeye, Waziri pamoja na Katibu Mkuu. Hakuna haja ya kusubiri mpaka bajeti fedha tumekwishatuma 1.3 billion kwa ajili ya utekelezaji. Mheshimiwa Mbunge asimamie mradi ule uanze haraka sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. RICHARD M. NDASSA (K.n.y. MHE. KISWAGA B. DESTERY) aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutumia mtandao wa maji Magu kupeleka Tarafa ya Ndagalu, Kata za Shishani, Njinjinili, Kabila, Nkungulu, Ng’haya, Sukuma, Buhumbi na Mwamabanza zenye jumla ya vijiji 24?

Supplementary Question 4

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Mji wa Tunduma ni mji unaokua kwa kasi na kuna miradi karibuni miwili au mitatu inatekelezwa kwenye Mji wa Tunduma, lakini tangu imeanza kutekelezwa mpaka sasa hivi wananchi hawajaanza kupata maji ya uhakika na Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri pamoja wamekuwa wakiwapa tarehe kila wakati za kumaliza miradi hiyo.

Je, ni lini miradi hiyo itakamilika ili wananchi wangu wa Mji wa Tunduma waanze kupata maji safi na salama kwa wakati?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji kwanza nashukuru kuona Mheshimiwa Mbunge anakiri kwamba tunafanya kazi kubwa na ipo miradi ambayo tunaitekeleza katika Jimbo lake. Kikubwa ambacho ninachotaka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, sisi kama viongozi wa Wizara tumeshabainisha miradi ambayo ipo katika hatua mbalimbali kwa ajili ya ukamilishaji. Tumepanga katika wiki hii ya maji itakuwa siyo wiki ya mapambio, ni wiki kwa ajili ya kuzindua miradi yote ya maji, kwa hiyo Wakandarasi wajipange katika kuhakikisha wana-meet zile commitment tulizoziweka ili wiki hii ya maji tuweze kuzindua miradi mingi ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tunakualika katika kuzindua miradi yetu ya maji. Ahsante sana.