Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 15 2020-01-29

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. RICHARD M. NDASSA (K.n.y. MHE. KISWAGA B. DESTERY) aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutumia mtandao wa maji Magu kupeleka Tarafa ya Ndagalu, Kata za Shishani, Njinjinili, Kabila, Nkungulu, Ng’haya, Sukuma, Buhumbi na Mwamabanza zenye jumla ya vijiji 24?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Magu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji Magu Mjini ambao tayari umekamilika, una uwezo wa kuzalisha maji kiasi cha lita milioni 7.25 kwa siku, ukilinganisha na mahitaji ya sasa ya lita milioni 3.54 kwa wakazi wa Magu Mjini na Vijiji vya Kipeja, Sagani, Nyashimba na Ilungu. Hivyo Mradi huu una ziada ya maji ya lita milioni 3.71 kwa siku kwa sasa kutokana na ziada hiyo, Serikali kupitia Programu ya lipa kwa matokeo yaani Programme for Results (P4R) itajenga miundombinu ya usambazaji wa maji kutoka kwenye Mradi wa Magu mjini kupeleka kwa baadhi ya vijiji vilivyopo tarafa ya Ndagalu ikiwa ni pamoja na Vijiji vya Misungwi, Kitongo, Lumeji, Buhimbi, Iseni, Nyang’hanga na Nyashoshi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha kuwa azma ya upatikanaji wa maji katika vijiji vingine vya Tarafa ya Ndagalu inapatiwa ufumbuzi wa kudumu, Serikali itahakikisha kuwa imetenga fedha katika bajeti ya Mwaka 2020/2021 ili vijiji vilivyobaki viweze kupata huduma ya maji kupitia Mradi wa Ziwa Victoria.