Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji kwa ajili ya Kyaka – Bunazi utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na shukurani za dhati kutoka kwa wananchi wa Wilaya ya Misenyi na Jimbo la Nkenge kwa mradi mkubwa wa maji ambao kwa mara ya kwanza sasa unaanza kutekelezwa, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; pamoja na ukweli kwamba mradi huu ni mkubwa lakini majibu yanaonyesha utatekelezwa katika bajeti ya Mwaka 2019/2020. Sasa katika kipindi hiki ambacho wananchi wanasubiri mradi huo mkubwa nini Serikali inafanya kuhakikisha maji yanaendelea kupatikana kwa uhakika ili wasipate tabu wakati wakisubiri mradi mkubwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili dogo; katika kikao changu cha wadau, wataalam waliniandalia taarifa nzuri na nikawaeleza wadau kuhusu Mradi wa aji ya Ruzinga lakini wadau wengi wakasema hapana Mheshimiwa unadanganywa, maji Ruzinga hayatoi.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari kufuatana na mimi ili twende kati ya Ruzinga ili tuone hizi fedha nyingi tunazopeleka tunafikiri maji yanatoka na hayatoki ili isije ikafika wakati mwingine ambao siyo muafaka wa kuuliza maswali kama haya twende pamoja anisaidie kutoa maelekezo ya Muarobaini wa matatizo hayo? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kiukweli amekuwa akifanya kazi kubwa sana katika Jimbo lake. Kitu ambacho nimhakikishie; mimi ni Naibu Waziri wa Maji, faraja yangu ni kuona Wanankenge wanapata maji safi na salama. Sasa nataka nimhakikishie baada ya Bunge tutafika na tukiona mradi ule ambao tumetoa fedha maji hayatoki tutamchukulia hatua Mhandisi wa maji pamoja na Mkandarasi ambae amepewa sehemu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kikubwa ambacho nataka kumweleza Mheshimiwa Mbunge ahadi ya utekelezaji wa mradi mkubwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na watalaam wetu wameshafanya usanifu ninachotaka kumhakikishia, katika kipindi hiki ili wananchi waweze kupata huduma ya maji timu yetu imegundua kisima kikubwa sana katika Kijiji cha Igayaza, tutatekeleza mradi wa haraka ili wananchi wake waweze kupata huduma hii muhimu sana ya maji. Maji ni uhai na sisi kama viongozi wa Wizara ya Maji hatupo tayari kupoteza uhai wa Wanakyaka. Ahsante sana.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji kwa ajili ya Kyaka – Bunazi utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa matatizo wanayoyapata wananchi wa Nkenge pia yanawapata wananchi wa Kigamboni. Je, Serikali ina mkakati gani mahususi wa kuhakikisha chanzo cha maji cha visima vya Kimbiji na Mpera kinakamilika ili wananchi wa Kigamboni, Mbagala, Chamazi, Temeke na maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam waweze kupata maji safi na salama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwa ufupi, hii ni Serikali ya Awamu ya Tano ikiahidi inatekeleza. Tumeshachimba visima zaidi ya 20 katika Kimbiji na Mpera na mpaka sasa tumeshamkabishi Mkandarasi kwa ajili ya uanzaji wa mradi wa Kigamboni ili wananchi wa Kigamboni waweze kupata huduma ya haraka. Kikubwa ambacho tunachotaka kumsisitiza Mkandarasi wa mradi ule aweze kufanyakazi kwa mujibu wa mkataba ili uweze kukamilika kwa wakati na wananchi wa Kigamboni na maeneo mengine waweze kupata huduma ya maji. Ahsante sana.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji kwa ajili ya Kyaka – Bunazi utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba niulize swali dogo la nyongeza. Najua mradi wa Maji Bunda ni wa muda mrefu na nimeushughulikia sana, hilo halina ubishi. Najua tatizo sasa hivi siyo maji kutoka kwenye chanzo kule Nyabehu, tayari sasa hivi maji yanakuja. Tatizo kubwa ni mtandao wa kuhakikisha wananchi wengi wa Bunda Mjini wapate maji safi na salama. Sasa, ni lini Serikali watahakikisha wanasambaza mtandao mkubwa wa maji na kuunga mkono juhudi zangu kwa kutenga fedha za Mfuko wa Jimbo kuwasaidia kutandaza huo mtandao ili wananchi wa Bunda kwenye kata zote 14 wapate maji safi na salama, ni lini?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Bulaya kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda atambue kwamba Serikali imefanya jitihada kubwa sana katika Jimbo lake la Bunda, tuna utekelezaji wa mradi zaidi ya bilioni 10, huo unaendana sambamba kabisa na utandazaji wa mtandao wa maji. Kikubwa ambacho ninachotaka kumhakikishia, Serikali hii ya Awamu ya Tano tutahakikisha kazi ile inakamilika kwa wakati na wananchi wake waweze kupata huduma hii muhimu sana ya maji.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji kwa ajili ya Kyaka – Bunazi utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 4

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri Mradi wa Maji wa Kata ya Sigino, Mheshimiwa Waziri alifika mwaka jana akaahidi kwamba wataalam wake watafika ndani ya siku 10 ili ule mradi uanze.

Naomba nifahamu hawa watalaam watafika ili wananchi wale wapate maji? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya tukutane basi baada ya Bunge ili tuweze kukutana na wataalam wetu na kuweza kuwaagiza haraka wafanye kazi. Ahsante sana.