Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 14 2020-01-29

Name

Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:-

Je, ni lini mradi wa maji kwa ajili ya Kyaka – Bunazi utaanza kutekelezwa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Balozi Dkt. Diodoras Buberwa Kamala, Mbunge wa Nkenge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika katika juhudi za kuboresha huduma ya maji katika Kata za Kyaka na Bunazi, Serikali ilibuni mradi wa maji ambao utawahudumia wananchi wa kata hizo. Usanifu wa mradi na taratibu za ununuzi wa Mkandarasi wa ujenzi wa mradi huo zimekamilika. Utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Kyaka-Bunazi umepangwa kutekelezwa katika mwaka 2020/2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi kuu zilizopangwa kutekelezwa kwenye mradi huo ni ujenzi wa tekeo la maji litakalojengwa katika mto Kagera eneo la Rubale, ulazaji wa bomba kuu urefu wa kilomita 1.5, mtambo wa kutibu maji na Tanki la kuhifadhia maji lenye lita milioni mbili litakalojengwa katika eneo la Kituntu. Mradi huu ukimalika unatarajiwa kuhudumia jumla ya wakazi wote wa kata za Kyaka na Bunzai wapatao 64,470.