Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Barabara za Mji Mafinga hazipitiki kwa mwaka mzima na kati ya kilomita 407 kwa mujibu wa DROMAS lami ni kilometa 5.58. Je, Serikali ipo tayari kuongezea fedha TARURA ili ijenge barabara za kupitika kwa mwaka mzima?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza na kabla ya swali la nyongeza ningependa kuwasilisha shukrani zangu kwa TARURA Mafinga na TARURA Iringa kwa jinsi ambavyo wanajituma kufanya kazi pamoja na mazingira ya uhaba wa fedha. Pia na Wakala wa Misitu Tanzania kwa maana ya shamba la Sao Hill ambao mara kwa mara tumeshirikiana nao kwa kutusaidia Greda na sisi halmashauri kujaza mafuta kusembua barabara zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nina maswali mawili ya nyongeza swali la kwanza kwa mujibu wa mgao wa fedha za mfuko wa barabara kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri mpaka hapa tulipo TARURA inapata asilimia 30 na TANROADS inapata asilimia 70 na wote wanashughulika na barabara ambazo ni za muhimu katika Taifa letu, lakini bado TARURA barabara zao ndiyo zinazobeba mazao zinabeba biodhaa, zinabeba mbolea.
Je, mbali ya hiyo kanuni Serikali iko tayari kutafuta namna nyingine ya kuwa chanzo maalum cha kuiwezesha TARURA ifanye kazi zake kwa ufanisi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili Mji wa Mafinga Mjini unakuwa kwa kasi na ndiyo kitovu cha uchumi wa mazao ya misitu katika Wilaya Mufindi na Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

Je, Serikali iko tayari japo kuiangalia Mafinga kwa macho mawili ili kusudi miundombinu yake iweze kuboreshwa na hivyo mchango wake katika uchumi wa Taifa ukaongezeka?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tumekuwa na changamoto ya mgao wa fedha na tumepokea pongezi kwa niaba ya Serikali kwa kazi nzuri ambayo inafanyika na TARURA na nchi karibu kila halmashauri. Changamoto kubwa ni ufinyu wa bajeti na upungufu wa fedha ambao upo inapelekea changamoto hizo kuendelea kuwepo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mambo mengine kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge jambo hili la mgao wa fedha linafanyiwa kazi kuna Kamati maalum iliundwa naifanyia kazi na Waheshimiwa Wabunge humu ndani walishatoa maoni mbalimbali kutafuta chanzo mbadala, pia kuangali formula ambayo itatumika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, pamoja na mambo mengine tutaendelea kufanya pia kazi hiyo huu mchakato tutakamilisha na ikishindikana kupata mgao wa fedha hizi au hata 50 kwa 50 basi tuangalie vyanzo vingine vya kusaidia barabara zetu ziweze kupitika. Ni kweli kwamba barabara hizi ni muhimu sana ndipo walipo wananchi wengi, huduma za kijamii nyingi tunajua zinapitika wakati wote na hasa wakati huu wa mvua.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili Mheshimiwa Mbunge anataka kujua kama Serikali inampango wa kuboresha Mji wa Mafinga. Niseme tu kwamba Serikali ina mpango wa kuboresha maeneo yote ya Miji ikiwepo Mafinga Mjini pindi tukipata uwezo wa fedha wa kutosha na kuhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi hiyo itafanyika kwenye eneo lake ili uchumi uweze kukua na huduma iweze kupatikana kwa haraka na kwa gharama nafuu, ahsante.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Barabara za Mji Mafinga hazipitiki kwa mwaka mzima na kati ya kilomita 407 kwa mujibu wa DROMAS lami ni kilometa 5.58. Je, Serikali ipo tayari kuongezea fedha TARURA ili ijenge barabara za kupitika kwa mwaka mzima?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona, barabara ya kutoka Iringa Mjini kwenda Wilaya ya Kilolo kilometa 133 ambayo kuna kipande cha Jimbo la Kalenga napo kuna changamoto ya barabara mvua zimenyesha barabara nyingi zinakuwa hazipitiki vizuri wananchi wanapata adha na mazao yao yanashindwa na ni ahadi ya Rais ambayo alitoa kwamba kufikia 2020 itakuwa imetengenezwa.

Ni lini sasa Serikali itahakikisha barabara hii inatengenezwa na wananchi wanapita bila matatizo?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge watakubaliana na mimi kwamba kipindi hiki tumepata mvua myingi sana na uharibifu wa miundombinu umekuwa ni mkubwa sana, sisi
kama Seriikali tumejipanga kuhakikisha kwamba tunakwenda kufanya urejeshaji wa miundombinu hii. Niseme tu kilometa 4217 hadi Desemba zimekuwa na hali mbaya hizi ndiyo barabara katika nchi tunaendelea na uratibu nimuombe Mheshimiwa Mbunge avute subira tumeshatambua maeneo yote yenye shida na tunahitaji fedha za ziada kwenda kufanya marejesho ya miundombinu ya barabara.

Kwa hiyo, wananchi wavute subira sisi kama Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi kwa kushirikiana na wenzetu upande wa Serikali za Mitaa kwa maana TARURA tunafanya uratibu wa pamoja ili tuhakikishe kwamba tunaenda kufanya uridhishaji maeneo mbalimbali ya nchi maeneo ambayo yameharibiwa na mvua, ahsante sana. (Makofi)

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Barabara za Mji Mafinga hazipitiki kwa mwaka mzima na kati ya kilomita 407 kwa mujibu wa DROMAS lami ni kilometa 5.58. Je, Serikali ipo tayari kuongezea fedha TARURA ili ijenge barabara za kupitika kwa mwaka mzima?

Supplementary Question 3

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ni miongoni mwa halmashauri ambazo zilielekezwa kuhamisha Makao yake Makuu ya halmashauri kutoka Mjini kwenda kwenye maeneo yake ya utawala, lakini kuna changamoto kubwa sana ya barabara haswa kwa wananchi wa Tarafa ya Bungu barabara ya kutoka Makuyuni Kwemshai na barabara ya Makuyuni, Zege Mpakayi.

Je, Serikali iko tayari sasa kuwa na mkakati maalum wa kusaidia uboreshaji wa miundimbinu ili wananchi hawa waweze kufika kiurahisi kwenye maeneo ya Makao ya halmashauri mpya zilizoanzishwa?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa kwanza nimpongeze kwa namna anavyohangaika na barabara za eneo lake na nimshukuru alinipa ushirikiano wa hali ya juu nilivyotembelea maeneo haya na maeneo mengine ambayo hakuyataja.

Mheshimiwa Naibu Spika, na niseme tu labda ni kwa kutoa kumbukumbu sahihi kwa mvua ambazo ambazo ziliathiri Mkoa wa Tanga zilikuwa ni kubwa sana kiasi kwamba urejeshaji wa maeneo ambao tumeyafanya hadi sasa tumetumia bilioni 7.8 kurejesha eneo la Tanga peke yake kwa mvua za mwezi Octoba peke yake na nikubaliane na yeye kwamba sasa tumefanya tena kwenye uratibu huu wa mvua zilizonyesha kuanzia Octoba kuja Januari kwa upande wa Tanga pia kumbukumbu kwamba kuna mahitaji makubwa ikiwepo maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge umeyataja.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tumetambua maeneo yote yenye shida hizi ikiwepo maeneo uliyoyataja na tunafanya utaratibu wa kuwa na fedha tena kama tulivyofanya Awamu ya I ya mvua za mwezi Octoba tutakwenda kufanya kazi kubwa kufanya marejesho ya maeneo haya ambayo nayataja kwa sababu nafahamu eneo la kwako pia ndiyo limekumbwa na maporomoko ya udongo wananchi wamepata athari kubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tunatambua hivyo na tutakuja kufanya uharaka wa kurejesha maeneo hayo uliyoyataja,ahsante sana.